MASIGNCLEAN101

Nadharia zinazo jadili Chimbuko la Fasihi

Nadharia zinazo jadili Chimbuko la Fasihi
citylab
Monday 1 February 2021

 

Chimbuko la Fasihi
Kuna nadharia kuu nne za chimbuko la fasihi.

Nadharia ya kwanza, ambayo baadhi ya watu wameiita ya “kidhanifu”, yaani yenye fasihi ni
Mungu. Nadharia hii ni kongwe sana, ilikuwako hata kabla ya kuzaliwa Kristo. Mathalani, Wayunani
wa kale huko Ulaya walikuwa na Miungu wa ushairi na muzingi waliowaita Muse, ambao yasemekana
ndio waliowapa watunzi muhu au kariha (msukumo wa kiroho, kinafsi na kijaziba (inspiration) wa
kutunga. Maelezo ya wafuasi na nadharia hiyo yanadai kwamba Mungu ndiye msanii mkuu.

Kauumba ulimwengu kwa usanii wa ajabu. Mwanadamu pia ni zao la sanaa ya Mungu. Hivyo uwezo
wa mwanadamu wa kubuni kampa Mungu, ambaye ndiye msanii mkuu.

Maandishi ya wasomi wa kale wa Kiyunani, hasa Hesiod na Plato, yanaanzia kwenye imani hii.
160Kwa mujibu wa nadharia hii, fasihi imekuwapo tangu kuwapo kwa mwanadamu duniani,
haikugunduliwa au kutokea katika kipindi Fulani tu cha maendeleo ya mwanadamu, bali ni zawadi
ya Mungu kwa wanadamu.

Dosari kuu ya nadharia 

hii ni kwamba inachanganya imani ya taaluma. Ni nadharia isiyo na
uthibitisho au ushahidi kisayansi, hivyo ni ngumu kuijadili kitaaluma.

Dosari nyingine ni kwamba nadharia hii inatafuta chimbuko la vitu vya kitamaduni nje ya maisha ya
mwanadamu, na nje ya dunia hii, na hivyo kukanusha athari ya mazingira na mapambano ya
mwanadamu katika kumuumba mtu au utamaduni wake.

Katika taaluma ya fasihi ya Kiswahili, nadharia hii inajitokeza katika kazi za Nkwera (1976) na
Ramadhani (Mulika 3:5).

Nkwera anatwambia:
Ulimwengu, mbingu na dunia na vitu vyote vilivyomo ni Sanaa Kuu ya Mungu. Siyo sanaa nzima lakini, bali ni
sehemu tu yake inayotupwa kwenye kioo kwa wakati moja (!) na mwanadamu akaiangalia. Na kila nukta
aangaliapo katika kioo hicho huona ufundi mpya, ufundi unaomwajabisha zaidi kila dakika.Sanaa isiyo lugha ya
kuieleza kikomo. Kila siku Mwanadamu anatalii, anaongelea na kuranda ndani ya hiyo sanaa, mwenyewe akiwa
sehemu ya hiyo sanaa, apate kuiweka sanaa hiyo nzima katika ukurasa mdogo wa akili yake. Ataweza
wapi?(uk.45).
“…..Fasihi ni sanaa inayoambatanishwa na lugha. Ni moja tu, nayo inafanya duara kubwa. Huanzia
kwa Muumba, humfikia mtu katika vipengele mbalimbali, cha mwisho akiwa darasani, halafu
huungana tena na Muumba wake ‘(uk.62).

Nadharia ya pili inayoelezea chimbiko la fasihi ni ile inayyodai kuwa fasihi na sanaa zilitokana na
sihiri. Istilahi ya “sihiri” hapa ina maana ya uwezo au nguvu ya kimiujiza inayotumiwa na watu
kusababisha matokeo fulani. Katika lugha ya Kiingereza istilahi inayotumika ni magic.
Watetezi wa nadharia hii hudai kuwa chimbiko la fasihi na sanaa ni haja ya mwanadamu ya
kukabiliana na kujaribu kuyadhibiti mazingira yake. Hata hivyo, katika hatua za mwanzo za

maendeleo ya mwanadamu, haikutimilika ipasavyo kwa kuwa uwezo wa kisayansi na kiteknolojia wa
mwanadamu wa wakati huo ulikuwa bado uko katika kiwango cha mwanzo. Hivyo, sihiri – au imani
katika miujiza – aghalabu ilichukua nafasi ya sayansi na ugunduzi . Fasihi na sanaa zilichipukakama
vyombo vya sihiri hiyo katika kujaribu kuyashinda mazingira. Kwa mfano wawindaji walichora
kwanza picha ya mnyama waliyetaka kumwinda kasha wakaichoma picha hiyo mkuki au mshale kwa
kuamini kuwa kitendo hicho kitatoke kuwa kweli watakapokwenda kuwinda. Nyimbo walizoimba na
maneno waliyonuizia wakati wa kufanya sihiri hiyo ndiyo ushairi wa mwanzo.

Dosari ya nadharia
hii ni kwamba inachanganya dhima na chimbuko. Kutumika kwa fasihi katika
sihiri hakuthibitishi kuwa sihiri ndiyo chimbuko lake. Sihiri ni amali moja tu kati ya amali nyingi za
wanadamu wa mwanzo zilizotumia sanaa na fasihi.

Nadharia ya tatu ya chimbuko la fasihi inadai kuwa fasihi imetokana na wigo (uigaji).
 Katika

nadharia hi, ambayo kwa lugha ya Kiingereza inatiwa mimesis, inaelezwa kuwa mwanadamu alianza
kuwa mbunifu kwa kuiga maumbile yaliyomzunguka, hivyo sanaa za mwanzo mara nyingi zilijaribu
kusawiri vitu vilivyomo katika mazingira , kwa mfano wanyama, ndege, miti, watu na kadhalika.
Nadharia hii vilevile ni ya kale, ilianzishwa na wanataaluma wa Kiyunani. Walioieneza zaidi ni Plato
katika kitabu chake cha Republic na Aristole katika Poetics. Aristotle (1958) anatuambia.


Plato anauhusisha wingo na dhana ya uungu. Anaeleza kuwa maumbile na vilivyomo ni wigo tu wa
sanaa chasili (archetype) za kiungu. Hivyo sanaa ya mwanadamu (hususan ushairi) ambao huiga tu
mambo hayo yaliyomo katika maumbile haiwezi kuwa na ukweli au uhalisi, kwa kuwa inaiga
maumbile ambayo nayo yanaiga kazi ya Mungu. Hivyo alishauri aina Fulani za ushairi zipigwe
marufuku kwa sababu zinapotosha ukweli.
Dosari ya nadharia hii ni kwamba inasisitiza mno uigaji na kusahau suala la ubunifu katika sanaa na
fasihi. Ni wazi kuwa kama watunzi na wasanii wangiga maisha na mazingira tu, sanaa yao ingepwaya
sana, na haingekuwa tofauti na picha ya fotografia au maelezo ya matendo ya mazingira na matendo
ya kila siku ya mwanadamu. Kwa kawaida watu hufurahia sanaa kwa kuwa inawapa kitu ambacho
hawakipati katika maisha na uzoefu wao wa kawaida.


Nadharia ya nne ya chimbuko la fasihi ni ile ya kiyakinifu. Nadharia hii, ambayo imejikita kwenye
fikra za Marx na Engels (rej. On Literature and Artm 1976) hudai kuwa mwanadamu ni zao la
maumbile asilia ya ulimwengu, kuwa mabadiliko ya mwanadamu kutoka katika hali ya unyama
kuingia katika hali ya utu yamechukua mamilion ya miaka, halikuwa tukio la siku au wiki moja tu.
Utamaduni, ikiwemo ugha ya fasihi , ni zao la mabadiliko hayo.

Nadharia hiyo inafafanua kuwa mwanadamu alianza kubadilika alipoanza kuwa mfanyakazi, kuzalisha
mali, na hivyo kubadili mazingira ya kimaumbile aliyoyakuta. Katika uzalishaji huo wamali,
mwanadamu ilibidi ashirikiane na wenzake. Hivyo alihitaji chombo cha kumwezesha kuwasiliana na
kuelewana nao. Logha ilianza kama njia tu ya kurahisisha mawasiliano hayo. Baadaye lugha hiyo
ikawa chombo cha sanaa yaani fasihi. Fasihi hiyo ya awali ilitumika kama zana ya uzalishaji, yaani
kwa lengo hilohilo la kuchapa kazi. Aidha, ilitumika kujenga hisia za kijinsia katika mahusiano ya
uzazi, ambao ndio uliokuwa msingi wa pili wa maisha ya jamii ya wakati huo. Kwa kadiri maendeleo
ya uzalishaji mali yaliyoongezeka na kumpa mwanadamu muda wa ziada wa kujiburudisha na
kustarehe kwa njia ya sanaa, fasihi ilianza kujitenga na kazi za uzalishaji , ikiwa ni sanaa ya burudani
au ya shughuli maalumu za kijamii, kwa mfano sherehe, ibada na kadhalika.

Dosari za mtazamo 
huu ni kwamba baadhi ya maelezo yahusuyo mabadiliko ya mwanadamu kutoka
katika usokwe kuingia katika utu, na hatua zake za mwanzo za kujenga utamaduni na lugha, bado ni
mambo ya kinadharia ambayo hayajathibitishwa kwa ukamilifu, japo ushaidi unazidi kukusanywa kila
uchao kutokana na ugunduzi wa saikolojia, sayansi za biolojia, kemia na kadhalika. Hata hivyo,
nadharia ya kiyakinifu inaeleka kubadilika zaidi kitaaluma kuliko nadharia ya kidhanifu na ile ya wigo.

Share This :
...