MASIGNCLEAN101

VIPENGELE VYA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI

VIPENGELE VYA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI
citylab
Friday 4 January 2019

VIPENGELE VYA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI
Yaliyomo
Fasili ya fasihifasili ya uhakikiVipengele vya uhakiki wa kazi za fasihi 
                       -Fani
                       -Maudhui
Fasihi ni sanaa inayo tumia lugha katika kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyo kusudiwa (Taasisi ya Elimu Tanzania, 1996). Haji (1983:30) fasihi ni sanaa itumiayo maneno ili kutoa picha halisi ya mwanadamu akiwa maishani mwake; mahusiano yake na viumbe wengine, migogoro yake na mazingira, shida zake, raha zake, matumaini yake na jinsi anavyopiga hatua katika maendeleo yake. Fasihi ni kazi ya sanaa itoayo maudhui yake kwa kutumia lugha ya kutamka au kuandika ili kufikisha ujumbe kwa jamii. Fasihi ni sanaa inayotumia lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii fulani (tunuzakiswahili.blogspot.com). Fasihi ni kazi ya sanaa inayotumia maneno katika kufikisha ujumbe kwa jamii, kuburudisha, kuonya, kukejeri, na hata kukashifu (www.shuledirect.com). Fasihi ni sanaa inayotumia ishara (maneno au matendo) kutoka picha halisi ya maisha kwa njia bunifu na inayofuata mpangilio maalumu na lugha ya kifasaha ili kuiathiri hadhira husika (Ntarangwi, 2004). Hivyo basi fasihi ni kazi ya sanaa itoayo maudhui yake kwa kutumia lugha ya kutamka au kuandika ili kufikisha ujumbe kwa jamii.
Uhakiki ni kitendo cha kutathimini, kueleza, kuainisha na kutoa maoni juu ya kazi fulani ya fasihi kwa kuongozwa na kaida maalumu (Ntarangwi, 2004). Uhakiki ni uchunguzi wa kazi ya kifasihi kwa makini na kwa utaalamu. Uchunguzi wa aina hii huchunguza uchanganuzi, fasiri, uelezaji, ufafanuzi, tathimini na utoaji wa kauli ya kijumla (Wamitila, 2002). Uhakikini utathmini, ufasili na uainishi wa kazi za fasihi, haumaanishi kutafuta makosa ya kazi hiyo(Peck & Coyle). Kwa hiyo, Uhakiki ni kitendo cha kuchambua, kutathmini na kuainisha kazi ya fasihi ili kuona ubora na udhaifu wa kazi hiyo kwa kutumia kaida au vigezo husika vya fani na maudhui.
Katika uchambuzi na uhakiki wa kazi za fasihi kuna vipengele vikuu viwili ambavyo ni; 
MAUDHUI
Maudhui ni kile kinachosemwa katika kazi ya fasihi (Ntarangwi, 2004). Maudhui ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa pamoja na mtazamo wa mwandishi juu ya mawazo hayo. Maudhui hujumuisha mawazo pamoja na mafunzo mbalimbali yaliyomsukuma msanii hadi akatunga na kusainii kazi fulani ya kifasihi (www.shuledirect.com). Maudhui ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa katika kazi ya fasihi. Hivyo tutaanza kwa kuchambua vipengele vya maudhui ambavyo hujumuisha dhamira, ujumbe, migogoro, mtazamo, na falsafa.
Dhamira ni ile jumla ya maana anayoivumbua mwandishi aandikapo, na jumla ya maana anayoitambua msomaji katika usomaji wake (Wamitila, 2002). Dhamira hutumiwa kurejelea mada ya kazi fulani au ujumbe au lengo la kazi hiyo. Kifasihi kuna aina mbili za dhamira yaani dhamira kuu na dhamira ndogondogo.
Dhamira kuu ni kiini cha kazi ya fasihi, ni wazo kuu, ni jambo linalomsukuma msanii kuandika kazi yake ili aweze kuufikisha ujumbe wake kwa hadhira. Dhamira ndogondogo, ni mawazo madogomadogo ambayo hujenga dhamira kuu.
Mifano ya dhamira ni kama zifuatazo kutoka katika kazi mbalimbali za kifasihi ambazo ni;- Kutoka katika Tamthiriya ya Amezidikilicho andikwa naSaid Mohameddhamira zilizomo ni kama vile Ulevi, mwandishi ameizungumzia katikauk 50 anasema “wanakunywa wisky…”. Na dhamira nyingine ni kama vile Umasikini na Matabaka uk 60. Tamthiriya ya Nguzo Mama iliyoandikwa naPenina Mhandoameelezea dhamira mbalimbali kama vile dhamira ya Ukombozi wa mwanamke, kama ilivyoelezwa na mwandishi kwa kumtumia “Bi Nane;Basi tusikilizane. Mnajua Nguzo Mama haiwezi kusimama mpaka tuivute kwa kamba”. Pia katika riwaya ya Kufirikamwandishi Shaban Robert ameonesha dhamira kuu ni Ukombozi wa kiutamaduni. Kiujumla riwaya ya kufikirikainajadili harakati zinazofanywa na Utu Busara za kupambana na tamaduni zilizopitwa na wakati. Pia mwandishi amejadili dhamira ndogondogo kupitia wahusika lukuki ambao amewatumia katika riwaya hii, Dhamira hizo ni kama zifuatazo: Suala la uongozi, Suala la ugumba na utasa,
Mgogoro ni hali ya kutokuelewana baina ya pande mbili yaani mtu na mtu, mtu na kikundi au mtu mwenyewe na nafsi yake. Migogoro ni mivutano na misuguano mbalimbali katika kazi za fasihi. Migogoro inaweza kuwa kati ya wahusika, familia zao au matabaka yao.Migogoro hii inaweza kugawanywa  katika vipengele vifuatavyo; 
mgogoro wa nafsi, mgogoro wa kijamii, mgogoro wa kiuchumi  mgogoro wa kisiasa. Mfano mwandishiShaaban Robert katika riwaya yake yaKufikirika ameonesha migogoro mbalimbali kama vile mgogoro wa kiuchumi, kijamii, kisiasa, utamaduni na mgogoro wa nafsi. Tukianza na mgogoro wa kiuchumi, mwandishi ameonyesha jinsi nchi ya kufikirika ilvyoyumba kiuchumi kutokana na mali zote za nchi zilivyotumika katika kumtibu mfalme na malkia na mwishowe shughuli za nchi zilisimama (uk.8-12). Pia kuna mgogoro wa kijamii, mwandishi ameonyesha mgogoro wa mfalme na malkia kwa kukosa mtoto, kwakua walijiona hawana  umuhimu katika jamii ingawa walikua na mali nyingi. (uk.1-6). Katika kitabu cha Tamthiliya ya Amezidi kilicho andikwa na Said Mohamed kuna mgogoro kati ya Marina Zidi, ambapo Mari aliahidiwa mali nyingi na Zidi lakini hakutimiziwa. Mfano,Mari anasema, “….ziko wapi, kanzu mpya za kujimwaga? Ukasema mabegi sita yananingojea mimi… na manukato… na mambo kemkem ya kujipodoa….” (uk. 23).Pia mgogoro kati yaAme na Zidiunaojitokeza pale wanapogombania nyama, kwa mfano mwandishi anasema,”Nyama inawaanguka na wao wanavaana na kupigana….” (uk.70). Pia katika Riwaya yaKusadikika iliyo andikwa na Shaaban Robert, ameonesha migogoro mbalimbali kama vile, migogoro ya kijamii. Mfano wa migogoro ya kijamii ni mgogoro wa Sapa naSalihi uliotokea baada ya Sapa kuomba upofu kutokana na tamaa ya Salihi kutamani vitu vya Sapa (uk 30).Mgogoro wa Kisiasa.Huu ni mgogoro unaowahusisha wanaharakati wazalendo walioongozwa na karama dhidi ya serikali na viongozi wa nchi ya Kusadikika. Wanaharakati hao walihitaji mabadiliko na walichoshwa na uonevu wa viongozi wao, mgogoro huu ndio uliopelekea wananchi kuishia kifungoni pindi walipojitolea kudai mabadiliko. Migogoro mingine ni ule wa nafsia na  Kiuchumi.
Ujumbe ni funzo na maadili yaliyokusudiwa na mtunzi yaifikie jamii aliyoilenga kufikisha kazi yake ya fasihi.Katika riwaya yaKufikirika iliyoandikwa na Shaaban Robert kupitia dhamira mbalimbali zimeweza kutuibulia ujumbe ufuatao; Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Mfano wananchi wa kufikirika walikuwa na umoja katika kufanikisha ustawi wa nchi yao hali kadhalika watu wa kufikirika walikuwa na umoja na ushirikiano katika kufanikisha mfalme wao anapata mtoto.Kwenye upendo, umoja na ushirikiano hakuna vurugu na matatizombalimbali. Ustawi wa nchi ya Kufikirika umetokana na umoja na ushirikiano waliokuwa nao, naJamii isijiegemeze katika imani za kimila na kitamaduni tu bali iangalie upande mwingine. Hii inatokana na ukweli kwamba wanakufikirika walikuwa hawaamini masuala ya hospitali badala yake walikuwa wanaamini mambo ya kimila na kitamaduni. Pia katika Riwaya yaKusadikikailiyoandikwa naShaaban Robertameonesha ujumbe kama, Uongozi mbaya unachangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha maendeleo ya wananchikuwa na tamaa na viongozi kujali maslahi binafsi  kunapelekea hali duni ya wananchi walio wengi na Viongozi wanapaswa kuthamini haki za wananchi wanaowatumikia. Pia kutoka katika Tamthiriya ya Nguzo Mama iliyoandikwa naPenina Mhandoameonesha ujumbe mbalimbali kama vile,Umoja ni nguvu, Umuhimu wa ukombozi wa mwanamke, naUongozi bora ni chachu ya maendeleo.
Falsafa, kiujumla falsafa ni mchujo wa welekeo wa mawazo muhimu yajitokezayo kila mara katika kazi mbalimbali za msanii ( Senkoro, 2011). Falsafani imani na mwelekeo wa mwandishi kuhusu maisha. Kutoka Riwaya ya Kusadikikailiyoandikwa naShaaban Robert falsafa ya mwandishi ni ya“wema hushinda ubaya”, amedhihirisha hili kupitia mhusika Karama aliyechorwa kama mtu mwema dhidi ya Majivuno aliyechorwa kama mtu mbaya. Kwa taswira hii Karama amewakilisha wema wote katika jamii ya wasadikika na Majivuno anawakilisha wabaya wote katika jamii hiyohiyo. Piakatika kitabu cha Riwaya za Rosa Mistika, Mzingile na Nagona ziliyoandikwa na Kezilahabi falsafa yake ni “Maisha hayana maana”. Pia kutoka katika Tamthiriya iliyoandikwa na Penina Mhando ya Nguzo Mama mwandishi anaamini kwamba“Mwanamke ukimwezesha anaweza”.
Msimamo wa mwandishi, msimamo ndio uwezo wa kuwatofautisha wasanii wawili wanaotunga kazi za fasihi zilizo na kiini na chimbuko moja ( senkoro, 2011). Katika riwaya ya Kufikirikamwandishi Shaaban Robert anaonekana kuwa na msimamo wa kiyakinifu. Kwa mujibu wa mwandishi anaona katika kipindi cha sayansi na teknolojia mila na tamaduni za zamani zisipewe nafasi. Kutoka katika riwaya ya Kusadikikamsimamo wa mwandishi Shaaban Robert ni wa kimapinduzi, kwani anaonesha jinsi jamii ilivyopaswa kujituma tena kwa ujasiri, kupigania haki na mabadiliko ya wananchi wote.  Katika tamthiriya ya Nguzo Mama  msimamo wa mwandishi, Penina Mhando ni wa kimapinduzi, kwani anajaribu kuiaminisha jamii na kuibadirisha kifikra kutoka kutomwamini na kutomthamini mwanamke na kuanza kujenga imani juu yao. Mfano amemchora mhusika Bi- Nanekama mtu mwenye msimamo na mpenda maendeleo.
FANI
Fani katika fasihi ni ule ufundi wa kisanaa anaotumia msanii katika kazi yake (Senkoro 2011). Fani ni ufundi wa msanii katika kuumba umbo la kazi ya fasihi kutokana na ubunifu wake. Fani ni ufundi ambao msanii anautumia katika kufikisha ujumbe kwa jamii. Katika fani msomaji anatakiwa kuzingatia;
Muundo au mtiririko(ploti) wa kaziMtindo alioutumia mwandishi katika kazi yakeLugha - mwandishi ametumia lugha namna ganiMadhariWahusika - jinsi mwandishi alivyo wasawili wahusika wakeUsimulizi wa kazi za fasihi
Wahusika ni binadamu wanaopatikana katika kazi ya kifasihi na ambao wanasifa za kimaadili, kitabia, kiitikadi na kifalsafa ambazo hutambulishwa na wanayoyasema (mazungumzo) na wanayoyatenda (matendo) (Wamitila, 2002). Mhusika katika fasihi ni kiumbe cha hadithini kilichobuniwa na msanii ili kuendeleza hoja na maudhui yake katika kazi yake (Ntarangwi, 2004). Wahusika ni viumbe hai au visivyo hai ambavyo vinawakilisha watendaji halisi katika maisha ya kila siku ya jamii husika katika kuonyesha wasifu wa ndani na nje kama vile hali ya kusononeka mhusika, furaha au tabia fulani katika jamii inayotuzunguka. Hivyo wahusika huelezea hali halisi ya maisha ya jamii. Iwe mitaani, iwe sehemu za kazi, iwe shuleni na kwingineko ambako kunahusisha mikusanyiko ya watu wa tabia tofauti tofauti.Mhusika husaidia katika kuendeleza mada nzima anayoizingatia msanii hususa kwa kufululiza vitushi na visa mbali mbali katika kazi ya msanii ili kuwafikia wasomaji au wasikilizaji wake. Mhusika hupewa maneno, dhana, na hulka ambazo ni muhimu katika kujenga hadithi, dhamira, na maudhui ya kazi ile. Wahusika wanakusudiwa kutenda matendo, tabia au matukio halisi katika mazingira halisi. Wahusikawamegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni wahusika wakuu na wahusika wasaidizi. 
Wahusika wakuuni wale wanaobeba dhamira kuu katika kazi ya fasihi. Hawa ndiyo vipaza sauti vya mwandishi. Wahusika hawa huonekana kuanzia mwanzo wa hadithi hadi mwisho wake. Wahusika wadogoau wasaidizi ni wale ambao wanajitokeza hapa na pale katika kazi ya fasihi ili kukamilisha ulimwengu wa kazi hiyo. Wahusika hawa hutumiwa na mwandishi katika kukuza dhamira. Wahusika wadogo wamegawanyika katika aina mbalimbali. Wakowahusika bapa,Mviringo,Kinyago, Jumui, Batili, Foili na wahusika Kikalagosi.
Mfano katika Riwaya ya Kufikirikamwandishi Shaaban Robert amewatumia wahusika mbalimbali katika kuibua au kuunda dhamira zake. Baadhi ya wahusika aliowatumia ni kamaMfalme, huyu alikuwa ndiye kiongozi au mfalme wa nchi ya Kufikirika ambaye aliongoza vema na alikuwa mtu mwenye huruma na upendo na watu wake. Hali kadhalika mfalme alikuwa ni jasiri na mzalendo aliyepigania haki. Malkia, huyu alikuwa ni mke wa mfalme ambaye pia alikuwa anasumbuliwa na tatizo la utasa, ni mwanamke mvumilivu na mwenye subira, hivyo mwandishi kwa kumtumia mhusika Malkia ameibua dhana ya utasa na uvumilivu. Utu busara ujinga hasara, ni mhusika aliyeibua dhamira nyingi katika riwaya hii ya kufikirika, alikuwa ni mtu makini na mwenye upeo mkubwa katika kufikiria mambo. Huyu ndiye aliyetabiri kuzaliwa kwa mtoto wa mfalme, baadaye akawa mwalimu wa mtoto wa mfalme na baadaye akajiingiza katika ukulima (uk 49).Pia katika Tamthiliya ya Nguzo Mamamwandishi Penina Mhando amewachora wahusika mbalimbali ili kufikisha ujumbe aliokusudia kwa msomaji. Wahusika hao ni kama vile, Bi-Piliambaye alikuwa ni mpishi wa pombe, ni mpenda maendeleo na pia ni mke wa Sudi na mlezi wa familia. Bi-Nne huyu ni mhusika mkuu, ni mwenye wivu asiyependa maendeleo ya wenziwe, na ni mwenyekiti wa kamati ya mashauri. Bi- Naneni msomi, ni mpenda maendeleo, na ni mvumilivu. Kitabu kingine ni Riwaya yaAmezidi mwandishiShaaban Robertamewatumia wahusika kama, Ame na Zidihawa ni wahusika wakuu katika kazi hii. Wahusika wengine wadogowadogo niMari, Joice, na Jane.Kutoka katika tamthiliya ya Kwenye Ukingo Wa Thimkilicho andikwa naIbrahim Hussein yeye amewatumia wahusika wafuatao ili kufikisha ujumbe kwa wasomaji wake, Abert naMarther ambao ni wahusika wakuu katika tamthiliya hii na wengine wadogowadogo ni kama vile;- Kriss, George, Ridia, Jine,  naStella.
Muundo hutokana na umbo na mpango wa kazi ya fasihi; kwa hiyo hapa ndipo tutapata katika ushairi wa Kiswahili, mashairi yenye miundo mbalimbali iainishwayo na idadi ya mistari (vipande/mishororo) katika kila ubeti, mathalani mashairi ya uwili, utatu, unne  (Senkoro, 2011)Muundo katika kazi ya fasihi muundo ni mpango na mtiririko wa kazi hiyo kwa upande wa visa na matukio (Senkoro 2011). Muundo ni namna matukio katika kazi ya fasihi yalivyopangwa na kuleta mtiririko wa kazi husika ya fasihi. Muundo ni mtiririko wa kazi ya fasihi kwa upande wa visa na matukio. Kinachozingatiwa hapa ni jinsi mwandishi alivyopanga kazi yake  mfano sura na sura, kisa na kisa au tukio na tukio. Muundo unaweza ukawa wa aina zifuatazo.
Muudo sahili.- Muundo wa moja kwa mojaMuundo wa urejeshi-Muundo wa kuanzia mwisho-kati-mwanzo au kinyume chake.Muundo wa duaraMuundo changamani- huwa na matukio/hadithi tofauti tofauti ndani ya hadithi au kisa kimoja.Muundo mpalaganyiko.
Hivyo katika riwaya yaNagona mwandishi E. Kazilahabi ametumia muundo wa “Rejea” ambapo mwandishi ameanza na kisa cha mbele katika kazi yake. Kutoka katika Tamthiliya ya Nguzo Mama mwandishi ametumia muundo wa “moja kwa moja” (sago) ambapo amepanga matukio au visa vyake kwa mtiririko kutoka onesho la kwnza hadi la nne. Kitabu kingine ni kile cha Kufikirikamwandishi ShaabaRobert ametumia muundo wa “moja kwa moja” ambapo amesimulia kitabu mwanzo hadi mwisho. Kwa kuigawa kazi yake katika sehemu ndogondogo, kwakuzipa vichwa vya habari kama vileMfalme, Waganga,Matokeo ya utabiri,Mtoto wa mfalme na Kafara. Pia sura ya tano ameigawa katika sehemu kuu mbili na kuipa jina la Baraza na Gereza.
Mtindo, katika kazi ya fasihi ni ile nama mbayo msanii hutunga kazi hiyo na huipa sura ambayo kifani na kimaudhui huainisha kanuni au kawaida zilizofuatwa kama ni zilizopo (za kimapokeo) au ni za kipekee (senkoro 2011). Mtindo ni upekee wa uundaji wa kazi ya fasihi na hutofautiana baina ya msanii mmoja na mwingine kulingana na hisia za msanii huyo. Utofauti huo unaweza kujitokeza kwenye matumizi ya nafsi, uteuzi wa msamiati, mwanzo na mwendelezo wa kazi yake, usimulizi wa mwandishi, uchanganyaji wa tanzu mbalimbali za fasihi, kama vile kuingiza kipengele cha wimbo katika kazi ya fasihi andishi. Katika Tamthiliya ya Nguzo Mama mwandishiPenina Mhandoametumia mtindo wa “majibizano (dialojia) (uk 36- 37), mtindo wa “monolojia” (uk 13 na35), mtindo wa nafsi zote tatu mfano;Nikianza kuyasimulianafsi ya kwanza,Nawewe wajua kupikanafsi ya pili, na ile ya tatu ambayo niWakaanza kuinua. Katika Riwaya yaKufikirika MwandishiShaaban Robert katika kazi yake hii ametumia mtindo wa “masimulizi” yaani amesimulia matukio yote katika mtiririko unaofaa, pia “nafsi zote tatu zimetumika”, hali kadhalika mwandishi ametumia “ushairi” (uk 18-19). Pia ametumia mtindo wa kutoa maana ya meneno magumu mwishoni. Pia katika Riwaya yaKusadikika MwandishiShaaban Robertametumia mitindo mbalimbali katika kazi hii kama vile, ametumia “maswali” hasa katika sehemu ya mwisho ya kitabu, ametumia “diolojia” kati ya Sapa na Salihi (uk. 29), ametumia “masimulizi” kwa kiasi kikubwa, na matumizi ya “nafsi ya pili na tatu umoja na nafsi ya tatu wingi” sehemu kubwa ya kazi yake.
Mandhari huwa ni sura ya mahali hususa jinsi panavyoonekana katika hali halisi ya maisha. Mtunzi anaweza kutumia mandhari kueleza mazingara halisi ya kisa anachosimulia katika kazi yake. Mathalani, mtunzi anaweza kutuchorea mandhari ya pwani kwa kushughulikia vitu kama vile upwa na ziwa, minazi, nyumba za makuti n.k. Jambo hili huleta hali ya ufasaha katika utunzi (Ntarangwi, 2004). Mandhari ni ile arki au elementi ambayo hutufichulia wapi na lini ambapo matukio fulani yalifanyika (Wamitila, 2002). Mandhari ni mahali ama wakati tukio la kifasihi lilivyobuniwa na kutendeka na msanii na hivyo hufanikiwa kujenga hisia ya msomaji au msikilizaji ama mtazamani kulingana na kazi yake ya fasihi aliyoiandaa. Mandhari ni sehemu ambayo kazi ya fasihi ilitendeka, inatendeka au itatendeka. Kazi ya fasihi iwayo yote ile lazima iendane na mandhari husika. Aidha mada au jambo linalozungumzwa sharti iendane na sehemu au mahali ambapo tukio hutokea. Madhari hutumika kulejelea wakati na sehemu matukio ya msuko hutokea. 
Kwa mfano katika riwaya ya kufikirikamwandishi Shabani Robert ametumia mandhari ya kufikirika, kwani hata nchi inayozungumziwa ni ya Kufikirika, pia nchi zilizopakana na nchi ya Kufikirika nazo ni za kufikirika. Pia mwandishi ametumia muktadha halisi kama vile Gerezani, Nyumbani kwa Mfalme, Bustanini (uk 1) na Shambani. Kupitia mandhari hizi mwandishi, Shabani Robert ameibua dhamira mbalimbali.Katika kitabu chaKusadikika mwandishi ametumia mandhari ya Kufikirika ambayo haiwezi kuonekana kwa macho ya kawaida kwani ni nchi inayoelea angani. Pia ametumia mji wa Sadiki na mipaka au pande sita zinazopakana na nchi hii za Kaskazini, Mashariki, Kusini, Magharibi, Ardhini na Mbinguni. Pia kitabu  cha tamthiliya yaNguzo Mamamwandishi ametumiamazingira halisi kwani ni ya kijijini.
Matumizi ya lugha ni namna ambavyo msanii ameteua na kupangilia tamathali za semi kama sitiari, tashbiha, takriri, tashihisi na tafsida,  methali, misemo, taswira,nahau, lugha za kigeni na kadhalika. 
Matumizi ya lugha, hujumuisha jinsi mtunzi alivyotumia lugha katika kuwasilisha kazi yake. Matumizi ya lugha hujumuisha misemo, nahau, methali na tamathali za semi. Mifano ya matumizi ya lugha kutoka kazi mbalimbali za kifasihi ni kama ifuatayo;- Katika kitabu cha riwaya cha Kufikirikamwandishi ametumia lugha ya,  Methali,methali zilizotumika katika riwaya hii ni kama vile, nyumba ya mgumba hainamatanga (uk 5), mwenye haya hazai (uk 6), asiye kubari kushindwa si mshindani” (uk 27).Kutoka katika kitabu cha Kusadikikamwandishi Shaaban Robert  ametumia methari kama, Kitanda usichokilalia hujui Kunguni wake,  Msiba wa kujitakia hauna kilio, Lila na fila hawatangamani. Pia katika tamthiliya yaNguzo Mamamwandishi ametumia methari zifuatazo katika kazi yake,Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu (uk 30), Lamgambo likilia lina jambo (uk 4), Aso mwana aeleke jiwe (uk 4). Misemo, Katika riwaya ya Kufikirika misemo iliyotumika ni kama ifuatayo;- Dunia haifichi siri (uk 23), maisha ni kama kuwa katika bahari ( uk 24). Kitabu cha Nagonamwandishi ametumia misemo kama Fikra hufumba mboni za urazini (uk 14) Pia kutoka katika tamthiliya ya Nguzo Mamamwandishi ametumia misemo kama, Ukilikoroga pumba nakula utalila (uk 26), Utakufa kibudu (uk 23), Akachanganya ulimi (uk 57). Katika kitabu cha Kusadikika  mwandishi ametumia misemo mbalimbali kama vile, kumtosa mshitakiwa katika bahari ya maangamizi. Tamathali za semi, haya ni maneno ambayo hutumiwa na wasanii wa fasihi ili kutia nguvu katika maana, mtindo na hata sauti katika maandishi au kusema. Pia tamathali za semi hutumika ili kupamba lugha au mazungumzo. Mfano katika riwaya yaKusadikika mwandishi Shaaban Robert ametumia tamathali mbalimbali kama zifuatavyo:- Tashibiha,katika riwaya hii tashibiha zilizojitokeza ni kama vile kichwa chake kilishindiliwa kama gunia (uk 29), Sauti ya waafrika ni kali kama ile ya radi (uk 6), Waliweza kunusa kama mbwa mwitu (uk 8), Akili yake kali kama wembe (uk 38), Maswali aliyamimina kama maji (uk 29). Kutoka katika kitabu cha Amezidi mwandishi ametumia tashibiha kama vile;Mkono wangu mrefu kama ule wa Shetani (uk 8). Kitabu chaMzingile kuna tashibiha kama Uogaji wangu haukuwa kama wa ndege (uk 7). Kitabu cha Nguzo Mamamwandishi ametumia tashibiha kamaAmevaa kama mkulima wa bara (uk 24), Wanasagwa kama mbuzi (uk 32), Anatembea kama amepigwa na bumbuazi (uk 8). Sitiari ni tamathali ya semi ambayo hulinganisha vitu viwili au zaidi bila kutumia maneno kama, au mithili ya. Katika tamthiliya yaAmezidi mwandishi Said Mohamed ametumia sitiari kama vile; Tuwe simba basi (uk 72). Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo, mwandishiKezilahabi ametumia sitiari kama vile “Huyu ni baba yako.” (uk.12) pia “Ujamaa ni mzuri.’ (uk.112) Takriri ni tamathali ya semi ambayo neon hujirudiarudia kwa lengo la kusisitiza jambo fulani. Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujomwandishi Kezilahabiametumia sitiari katika sehemu mbalimbali mfano “Haa! Haa! Haa!”(uk.12), “Mauti mauti” (uk.17). Pia katika tamthiliya yaAmezidi mwandishiSaid Mohamedametumia takriri mfano “mumu mumu” (uk.75), “Joto…joto...ndani joto na nje joto” (uk.36).
Tashihisi, hapa vitu visivyo na sifa walizonazo watu hupewa sifa hizo. Katika kitabu chaNagona mwandishi amezionesha kama ifuatavyo; Bonde la hisia (uk 16), bonde la mvi (uk 18). Kitabu chaVuta N`Kuvutemwandishi ametumia tashihisi zifuatzo; Nuru ya jua iliingia kwa hamaki chumbani mle na ilikashifu uchafu wote wa chumba kile (uk 49). Kitabu chaKufikirika mwandishiShaaban Robertametumia tashihisi zifuatazo, Sauti ya ndege waliokuwa wakiimba matawini kwa kuagana na mchana ilikuwa na simanzi masikioni (uk 1). Katika kitabu chaKusadikika tashibiha zilizotumika ni kama vile; Giza limezalo nuru na ufupisho uoni wa machoWakati una mabawa kama ndege (uk. 11). Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa FujoKezilahabi pia ametumia tashihisi mfano “kila jiwe walilokalia liliwaambia samahani umekalia bega langu.”(uk.32)
Mubalagha, ni tamathali ya semi ambayo hutia chumvi au hukuza jambo. Katika riwaya yaKufikirika mwandishi ametumia mbinu hii katika (uk 11) siku hiyo kuni, mkaa, na mafuta yote yalikwisha kwa kuchoma hirizi hizo, moshi mwingi uliruka juu ukatanda katika hewa kama wingu kubwa la mvua.
Matumizi ya lugha za kigeni, hizi ni lugha azitumiazo mwandishi katika kazi yake ya kifasihi ili kufikisha ujumbe na kumburudisha msomaji wa kazi yake. Mfano wa lugha hizo zilivyo tumika katika kazi za kifasihi ni kutoka kitabu chaAmezidi mwandishi ametumia maneno ya lugha ya kiingereza kama “How do you do? All right! (uk 60)”, Cheers! (uk 58), Entertainment (uk 49).Pia katika kitabu chaMzingile mwandishi ametumia maneno ya lugha ya kiingereza kama well done! (uk 40). Kitabu cha Nguzo Mama mwandishi ametumia maneno ya lugha ya kiingereza kama vile, My God, Degree. Aidha katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo mwandishi Kezilahabi ametumia lugha ya Kiingereza, mfano “Welcome back” (uk.88). “Security (uk.89 - 90).” Snow cap” (uk.62)
Pia lugha ya picha, waandishi wengi wa kazi za kifasihi hutumia lugha za picha ili kupunguza au kuficha baadhi ya mambo yasionekane dhahiri kwa mlengwa mwenyewe, au kuwakilisha tabia za watu katika jamii. Mfano kutoka katika kazi za kifasihi ni kama vile;- Katika kitabu cha Nagonamwandishi ametumia lugha ya picha kamaKamasi, na funza (uk 16), vinyesi (uk 19), nyuki (uk 56). Kitabu cha Mzingilemwandishi ametumia lugha ya picha kamaMjusi (uk 46). Kutoka kitabu cha Nguzo Mama mwandishi ametumia kamba, nguzo mama.
Kwa ujumla uchambuzi na uhakiki wa kazi mbalimbali za kifasihi humsaidia msomaji wa kazi husika ya kifasihi kuielewa au kupata mwanga fulani juu ya kazi husika aisomayo. Aidha kazi ya uhakiki hufanywa na mhakiki wa kazi ya fasihi ambaye ndiye hufanya kazi kubwa ya kuchanganua kazi mbalimbali za kifasihi ili ziweze kumrahisishia msomaji kuzielewa kwa ufasaha kazi husika.
                                                     
Share This :
...