MASIGNCLEAN101

Kidato cha Tano na sita Kiswahili 2 yote hii apa

Kidato cha Tano na sita  Kiswahili 2  yote hii apa
citylab
Sunday 28 October 2018


KIDATO CHA TANO $ SITA-KISWAHILI 2- MADA 1 : FASIHI KWA UJUMLA,MADA NDOGO -1; NADHARIA YA FASIHI


   MADA 1  :  FASIHI KWA UJUMLA

MADA NDOGO -1; NADHARIA YA FASIHI

Nadharia ni Imani au kanuni zinazofuatwa na watu Fulani au jamii katika kushughulikia  jambo Fulani mahsusi.

Nadharia za fasihi ni muongozo au kanuni zinazofuatwa na wataalamu (wanazuoni) mbalimbali katika kuteua fasili/maana halisi ya fasihi.

Fasihi ni nini?

Wataalamu mbalimbali wamefasili/Maana ya dhana ya fasihi, maana hizo ni kama zifuatazo:-

1.   Fasihi ni kioo cha jamii (maisha),fasili hii inamaana kwamba mtu anaweza akajitazama akaona taswira yake na akajirekebisha . Fasili hii ina udhaifu kwani kioo hakiwezi kumweleza  mtu jambo la kufanya ili hali yake iwe bora zaidi . Pia si sehemu zote takazojiona kwenye kioo(F.Mkwera , 1978)

2.   Fasihi ni hisi,Fasili hii ina maana kuwa lazima pawe na mguso fulani wa wahusika ndipo mtu aweze kuandika na kueleza jambo fulani,’Sengo na kiango  Wanasema “hisi ni kama kuona njaa, baridi, joto, uchovu pengine kuumwa. Hapa swali la kujiuliza ni kwamba, je fasihi ina maana moja kati ya hiyo? Uamuzi wa kutenda jambo huja wakati umeguswa?. Je hizo hisia ziko wapi? Je mtu ambaye haguswi  sana moyoni hawezi kuwa mwanafasihi  mashuhuri? Je mwanamuziki ambaye huusifu uzuri wa mwanamke anaguswa moyoni? Je mwandishi kama Shaban Robert,  E. Kazilahabi wameguswa mara ngapi? Vile vile kivipi waguswe Zaidi ya wengine?  (Sengo na Kiango) hivyo bado fasili hii ina udhaifu

3.   Fasihi ni mwamvuli wa mtu na jamii na utu na maisha ya hadhi na taadhima.Fasihi  hii ina maana kwamba mwamvuli humkinga mtu katika mvua na jua na fasihi huhifadhi na kukinga amali za jamii zisiharibike maana hii ni nzuri kwani inasisitiza utunzaji wa kile kizuri kwa maana kuwa jamii inachambua kuwa makini na kuona amali za jamii zinazohifadhiwa. Lakini swali la kujiuliza ni  kwamba jamii itasaidiwa?

Jamii haitulii kama maji katika mtungi  bali hubadilika mara kwa mara kutokana na nguvu za migongano, hivyo kitu kipya huzaliwa na cha zamani hufa kwasababu jamii haitulii, hivyo hakuna haja ya kuhifadhi amali za jamii chini ya mwamvuli. Zipo mila na desturi zilizohifadhiwa na makabila mengi ambazo hazina nafasi leo. Hali ya mabadiliko ya jamii kutokana na siasa, utawala, uchumi, elimu, sayansi na teknolojia vyote hivi katika maendeleo vitatoboa mwamvuli na kuziharibu amali zilizohifadhiwa (Sengo na Kiango 1973)

4.   Fasihi ni sanaa ya uchambuzi wa lugha yoyote kadri inavyosemwa,inavyoandikwa na kusomwa,Hii ni kweli kuwa fasihi lazima itumie lugha kwani lugha ndicho chombo muhimu kitumiwacho na fasihi na si fasihi  tu bali taaluma zote hutumia lugha.Udhaifu wa fasili hii ni kwamba maana hii imejikita katika uchambuzi wa Lugha kana kwamba hakuna vipengele vingine vinavyochambuliwa katika fasihi zaidi ya lugha na hii ni sawa na kusema umeme ni waya wa shaba kwa vile umeme umepita kwenye waya huo.Na hii ni si kweli kwani Hisabati,fizikia au historia si fasihi ingawa hutumia lugha.

5.Fasihi ni kielelezo cha hisia za mwandishi juu ya mambo yanayomwathiri yeye,kikundi au jamii nzima anamoishi na kwamba lengo lake ni kustarehesha au kufunza wasomaji.Fasili(maana) hii ni nzuri kwa ujumla lakini mapungufu yake ni kwamba imemuwekea mwandishi kama chanzo pekee cha uumbaji wa Sanaa na hasa akili yake pia maana hii imetokana  na falsafa ya kidhaanifu kwa kuhusisha uchambuzi wa mambo katika fikra bila  kutazama hali halisi ya maisha ya watu na vitu.

   6.    Fasihi ni chombo cha utetezi wa maslahi ya tabaka moja au jingine na kwamba mwandishi ni mtumishi wake anayejijua au asiyejijua atake asitake mwandishi huyu analengo au dhamira fulani anayotaka kuionesha.Wasomaji wanaweza kuyakubali au kuyakataa maudhui ya kazi yake na pengine jamii kufuatana na msimamo juu ya itikadi ya siasa (napengine amali za jamii) inayotawala kwa kipindi kile  na jinsi mwandishi anavyooanisha maandishi yake na itikadi hiyo.Fasili au maana hii ni nzuri sana kwani kwa kifupi ni kwamba fasihi ni mojawapo ya silaha nyingi zinazotumiwa na tabaka moja kutetea maslahi yake katika mapambano ya kudumu dhidi ya matabaka mengine.

Hitimisho kwa ufupi fasihi ni taaluma inayotumia Sanaa maalumu ya lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii inayohusika.Fasihi hutueleza uzuri wa maandishi au mazungumzo ambayo huonekana katika mashairi ,historia za maisha ya watu ,tenzi,hadithi za kusisimua na insha mbali mbali.

DHIMA YA MWANAFASIHI KATIKA JAMII

Maana ya mwanafasihi/mtunzi wa kazi ya fasihi

Ni mtu yeyote anayejishughulisha na uandishi au utungaji wa kazi za fasihi yaani fasihi andishi na fasihi simulizi.

DHIMA ZA MWANAFASIHI

1. .Kuelimisha jamii,Katika kuelimisha jamii mwanafasihi ;

  (a)Huchambua na kuchochea umma kuwafumbua macho,hufichua wazo au uchafu uliomo katika jamii,wagandamizaji hufichuliwa na wagandamizwao hupewa muongozo sahihi ili waitambue hali yao dhaifu.Mfano”Duka la Kaya”imechambua na kuchochea jamii ili iweze kupambana na hali mbaya ya maisha.

(b).Kupiga vita kwa hali na mali mazingira yote ya ujinga,maradhi,njaa na umaskini,Mfano mwandishi wa tamthiliya yaHawala ya fedhaanapambana na maovu kama vile ujinga na uvivu naNgoswe Penzi Kitovu cha Uzembe anajadili na kupiga vita uzembe  na mengineyo.

(c).Kukosoa jamii,Mwanafasihi anaikosoa jamii katika vipengele mbalimbali vya maisha.Mfano riwaya ya “ Vuta n’kuvute”inakosoa mila na desturi zilizopitwa na wakati “Raha karaha na Mashairi ya Chekacheka”mwandishi wa diwani hizi anaikosoa jamii ya Tanzania kwa mapana kama vile Uongozi mbaya,kukithiri kwa rushwa n.k.

(d).Kutia hamasa na kumfanya mtu asikate tamaa,Mfano S.Kandoro anaeleza hamasa ya wananchi waliokuwa wameungana kama “Siafu ili kumtoa nyoka pangoni katika shairi  liitwalo  ‘Siafu wamekazana’’.Mwandishi kwa hamasa amewaita waafrika njooni “au” kwetu ni kwa nini’.Hivyo ni wazi kuwa kazi hizi zinajitahidi kuendeleza mapambano dhidi ya ukoloni  mambo leo.

(e)Mwandisi anadhima kujenga misingi na fikra za usawa na demokrasia miongoni mwa umma wa wakulima na wafanyakazi,Mwanafasihi huyu huwatukuza wakulima na wafanyakazi pamoja na amali zao.

(f) Mwanafasihi hueneza mawazo na falsafa za jamii,Kwa mfano katika shairi na ngonjera za Mathias Mnyapala ametangaza sana siasa ya ujamaa na kujitegemea kwa kutumia ngonjera za UKUTA 1 & 2 vile vile riwaya kama vile mfaa na utu,njozi za usiku,ndoto yandaria ,jero si kitu n.k zimetangaza sana siasa ya ujamaa na kujitegemea hapa nchini Shaban Robert aliwahi kueneza falsafa juu ya kweli kwa kiasi kikubwa katika mashairi yake.

(g)Mwanafasihi hutoa mwongozo kwa kuikomboa jamii kutoka fikra mbovu za kugandamizwa,kunyonywa na kuonewa na kujikomboa ili iweze kupata haki na usawa,Mfano Riwaya ya kiimbila “Ubeberu Utashindwa” na tamthiliya ya E.Mbogo “Tone la Mwisho” G Husseni “Kinjekitile”

2.Kuburudisha,zipo kazi mbalimbali za fasihi zinazoburudisha.Msomaji au msikilizaji wa fasihi huburudisha yaani husisimsha mwili na akili na huvutiwa kihisia na kazi ya fasihi anayoisoma au kusikiliza.Tabia ya msomaji au msikilizaji huweza kujengwa kutokana na mafunzo na mifano bora ya matendo ya kuigwa anayoyapata katika fasihi.

3.Kuhifadhi na kurithisha amali za jamii,Amali za jamii ni pamoja na mila na desturi mtindo wa maisha,Imani, historia jiografia,visasili na visakale ni urithi wa maarifa ya kijadi kwa mfano tiba, sayansi ya kilimo,mbinu za uwindaji,ufundi wa aina zote n.k.Amali hizo huweza kuhifadhiwa na kuendelezwa na mwanafasihi na hivyo kurithishwa kwa vizazi vijavyo.

Kwa mfano tamthiliya yaKinjikitile inahifadhi mengi kuhusu hali ya maisha wakati wa ukoloni wa kidachi,Kurwa na Doto(1969) ni riwaya yenye kuhifadhi japo kwa kejeli,mila,desturi na itikadi za jadi za waunguja,Riwaya ya Bwana Mnyombokero na Bibi Bugonoka;Ntuhanalwo na Buliwali  iliyoandikwa na Anicet Kitereza imehifadhi mila,Imani,mtindo wa maisha,ufundi na taaluma mbalimbali za jadi za wakerewe mengi yaliyoeleza humo siku hizi hayapatikani popote isipokuwa katika riwaya hiyo, vile vile Mzishi wa Baba ana Radhi (1967) kinaeleza mila na desturi za wapangwa.

Watunzi hasa nyimbo na visasili hukoleza pia shughuli za kijadi za kiutamaduni kwa mfano Ibada,matambiko,sherehe,katika shughuli za aina hiyo nyimbo licha ya kuwa kiburudisho hubeba ujumbe wenye kuhusiana na tukio hilo.

4.Kudumisha na kuendeleza lugha,Kwa kadri lugha inavyotumiwa na kufinyangwa na watunzi ndivyo inavyokuwa na kupevuka.Maneno mengi yatumiwayo leo katika lugha mbalimbali yalibuniwa na kuenezwa na watunzi wa mashairi,riwaya,nyimbo na tamthiliya katika Kiswahili.Mifano mizuri ni maneno mengi yahusuyo Sanaa ya ushairi(vina, mizani, beti, mishororo, miwala, tathlitha, takhimisa, tarbia n.k)

Katika jadi ya ushairi wa kiswahili inadaiwa kuwa ushairi ulikua ni ghala ya maneno.Washairi walitumia maneno magumu au yasiyokuwa ya kawaida makusudi ili kuyahifadhi ysipote.katika tamaduni nyingine kazi hiyo hufanywa na kamusi pamoja na vitabu viitwavyo Hazina ya maneno kwa kuwa waswahili hawakuwa na kamusi kazi ya kuhifadhi maneno ilifanywa na ushairi.

DHIMA ZA MHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI

Uhakiki ni kazi au kitendo cha kuchambua au kufafanua kazi ya fasihi, kuweza kupata maadili na ujumbe uliomo katika maandishi  ya mwandishi asilia.

 AU  ni sayansi maalumu ya kuchambua na kuona ubora wa kazi hizo kwa kutumia vipengele mbalimbali vya fani na maudhui na kuangalia uwiano na uhusiano ama kuathiriana kwake. Uhakiki ni elimu na ujuzi wa kuipembua kazi ya sanaa inayohusika kimaudhui na kifani.

Uhakiki ni daraja ya juu ya maelezo ya kisanii yenye kuwalenga watu wa aina tatu:- wasomaji wa kawaida walio nyumbani na shuleni, waandishi asilia wa kazi za sanaa na wahakiki.Msomaji hupata mwongozo wa namna bora zaidi ya kumwezesha kuifahamu kazi ya sanaa kutokana na viwango tofauti vya uhakiki juu ya kazi za sanaa.

Mhakiki ni nani?

Mhakiki ni mchambuzi na mfafanuzi wa maandishi ya kisanaa hasa yale ya kifasihi. Ni jicho la jamii kwa vile anagundua mazuri yaliyomo katika kazi ya fasihi na pia ndiye anayeona hatari ya maandishi hayo kwa jamii. Mhakiki ni bingwa wa kusoma na kuchambua maudhui, maadili na ujumbe uliomo katika maandishi ya fasihi.

Ni mtu mhakiki anajihusisha na maandishi  ya waandishi asilia na hungalia kwa jinsi gani mwandishi anawakilisha hali halisi ya jumuiya ya watu. Kwa upande mwingine, mhakiki anashughulikia uwanja wa fasihi andishi pamoja na ule wa fasihi simulizi.

Sifa za mhakiki

·       Mhakiki anatakiwa ajue historia na mazingira yaliyomkuza mwandishi.Mhakiki ili aweze  kuifanya kazi yake vizuri anapaswa aelewe vema historia ya mwandishi na jamii yake inayohusika. Aelewe asili ya mwandishi, historia yake na utamadumi wake kwa ujumla. Kutokana na hali hii, mhakiki anaweza kuelewa kama mwandishi amefanikiwa kueleza ukweli wa maisha ya watu, yaani jamii inayohusika.

·       Mhakiki anatakiwa kuelewa historia na siasa ya jamii inayohusika.Hii itamwezesha kuyaelewa matatizo ya jamii hiyo. Mhakiki lazima aifahamu barabara jamii ambayo mwandishi aliandikia juu yake ili aweze kuandika uhakiki imara, ama sivyo atakwama na kuandika uhakiki dhaifu. Mhakiki anapaswa kuelewa historia ya watu ambao maandishi hayo yanawahusu, bila kuifahamu historia yao, itakuwa vigumu kwake kueleza bayana baadhi ya mambo ambayo mwandishi aliandika na kwa nini aliandika hivyo. Uhakiki wake ukisomwa na watu wanaoishi katika jamii hiyo si ajabu kusema yeye si mhakiki. Mhakiki huangalia jinsi gani mwandishi alivyoiwakilisha hali halisi ya jumuiya na historia ya watu hao.

·       Mhakiki  awe amesoma kazi mbali mbali za fasihi na siyo ile tu anayoifanyia uhakiki. Hii itamsaidia kuwa na ujuzi zaidi katika uwanja wa uhakiki.

·       Mhakiki anatakiwa asome tahakiki za wahakiki wengine katika uwanja wa fasihi na hata nje ya jamii yake ili kupata upanuzi zaidi katika kazi ya uhakiki. Hii itamsaidia kutoa uhakiki bora zaidi, kwani atakuwa amejifunza yale yaliyo mazuri na kuepuka makosa waliofanya wengine.

·       Mhakiki lazima awe na akili pevu sana ili aweze kung’amua mambo na akishayang’amua ayaandike kwa lugha rahisi ili mawazo yake yasomeke na kila mtu kwa urahisi, yaani atumie lugha ambayo itawatumikia wasomaji wake.

·       Mhakiki lazima ajiendeleze katika taaluma mbali mbali ili aweze kuwa na mawazo mengi ambayo yatamsaidia kuhakiki maandishi mbali mbali. Mhakiki hodari huichonga jamii yake kimawazo. Huiimarisha isitetereshwe au kupofushwa na waandishi wapotoshaji.

·       Mhakiki anapaswa kuwa na uwezo wa kuchambua mambo kisayansi bila kuonyesha hisia za wasomaji. Asiwe na  majivuno na awaheshimu  anaowahakiki  na anaotaka wasome uhakiki wake. Asichukie au kusifia tu kazi za waandishi kwa sababu zake binafsi bila kueleza ukweli wa kazi hiyo. Mhakiki ni rafiki wa mwandishi na wasomaji . Kwa hiyo, mhakiki ni lazima awe fundi katika kutoa hoja zake na lazima ziwe zinagonga, zenye kuibua udadisi na kuathiri.

·       Mhakiki anapaswa asiwe mtu wa kuyumbishwa na maandishi au maneno ya wahakiki au watu wengine. Tunatarajia aseme kweli kuhusu kazi hiyo. Uhusiano baina ya mhakiki na mwandishi usiathiri uhakiki wake.

   TAHAKIKI NI NINI?

Ni kitabu kinachotolewa na mhakiki kinachambua vitabu mbali mbali vya maandishi asilia. Tahakiki hutoa uchambuzi na uhakiki wa vitabu vya hadithi/tamthiliya/ushairi kwa kuzingatia vipengele vya fani na maudhui. Mfano wa tahakiki ni kama vile:- Senkoro(1988). Ushairi: Nadharia na Tahakiki. DSM: DUP,Kiango, Msokile na Sengo (1987), Uhakiki wa vitabu vya Fasihi Sekondari na vyuo. NPA, n.k.

Dhima ya mhakiki

·       Kuchambua na kuweka wazi mafunzo yanayotolewa na kazi za fasihi:Hapa mhakiki anatoa ufafanuzi wa kimaudhui wa kazi ya fasihi. Mhakiki husoma kwa uangalifu kazi ya fasihi.Baada ya kusoma kwa makini, hutafakari na kuchunguza maudhui, maadili na ujumbe ambao mwandishi amekusudia kuwafikishia wasomaji wake na jamii inayohusika.

·       Kuchambua na kufafanua picha za kisanii zilizotumika katika kazi ya fasihi:Mhakiki huwasaidia wasomaji ili wasishindwe kuyaelewa maudhui barabar kutokana na kukanyagwa na usanii. Matumizi, mathalani ya ishara ni baadhi ya mbinu ambazo zinaweza kumkanyaga msomaji ambaye hajapata utaalamu mkubwa wa kuchambua. Mhakiki wa kufichua ishara fulani ina maana kuwa amemsaidia msomaji kupata ujumbe kikamilifu.

Kuhusu matumizi ya picha, kwa kawaida, lugha ya picha ina mguso sana na huibua hisia aina na hata kuchekesha au kuwafanya watu walie machozi. Mhakiki sharti awaambie kwamba, matumizi ya picha ni mbinu mojawapo inayosaidia maudhui kuwaganda wasomaji. Picha inayochekesha, kufurahisha, kukejeli, n.k. Haikomei pale tu, kwani baada ya kucheka, n.k. msomaji huathiriwa sana kinafsi na aghalabu huachiwa mafunzo fulani. Hivyo mhakiki lazima achambue na kuyaweka wazi mafunzo yanayotolewa na picha hiyo.

·       Mhakiki ana dhima ya kumshauri mwandishi ili afanye kazi bora zaidi:Mhakiki anamfundisha mwandishi juu ya yale anayoyasema yanavyoweza kupokelewa na jamii. Humwonyesha msanii uzuri na udhaifu wa kazi aliyoisaini. Kitendo hiki humfanya msanii ajifunze mambo yapi ni mazuri na yapi ni mabaya kama anavyoelekezwa na mhakiki, na hivyo humfanya awe na nafasi nzuri ya kuirekebisha kazi hiyo atakapoishughulikia kazi nyingine. Kwa msingi huo, mhakiki anaweza kulaumu au kusifu/kumpongeza mwandishi wa kazi yoyote ya kisanaa.

·       Mhakiki ana dhima ya kumwelekeza msomaji ili apate faida zaidi kuliko ile ambayo angeweza kuipata bila dira ya mhakiki:Mhakiki huifunza jamii namna ya kupokea na kuifurahia kazi ya sanaa. Vilevile mhakiki huwasaidia wasomaji kuyabaini maandishi yaliyo sumu kwa jamii. Mhakiki lazima ayafichue maandishi hayo ili yasieneze sumu kwa jamii. Mhakiki lazima ayafichue maandishi hayo ili yasieneze sumu kwa jamii inayohusika.

·       Mhakiki ana dhima ya kukuza kiwango cha utunzi na usomaji wa kazi ya fasihi:Kutokana na ushauri anaopata mwandishi kutoka kwa mhakiki, humfanya awe makini zaidi wakati wa kushughulikia kazi nyingine.Vilevile wasomaji wanakuza kiwango chao cha usomaji kwa kufuata mawaidha ya mhakiki.

·       Mhakiki ana dhima ya kusema wazi kuhusu kiwango cha maandishi anayohakikiwa:Akisema wazi kwamba, maandishi hayo yako katika kiwango cha chini, mara mwandishi huyo asilia atakapoamua kutunga tena, atashawishika kuandika maandishi yaliyo kwenye kiwango cha juu zaidi. Na waandishi wengine watapatiwa msukumo wa kuandika maandishi yaliyo kwenye kiwango cha juu zaidi. Na waandishi wengine watapatiwa msukumo wa kuandika maandishi yaliyo kwenye kiwango cha juu pia. Na hivi ndivyo mhakiki anavyosaidia kukuza na kuendeleza maandishi ya taifa lake.

·       Mhakiki anatakiwa kuheshimu na kuthamini kazi za waandishi na kuzifanyia haki:Jamo la msingi (lazima) kuzingatia na kuwa, mhakiki afanyapo kazi yake huwa vitani. Mhakiki anapaswa kujua namna ya kuwanasa wasomaji bila wao kujitambua na kuwa na uwezo au kuchambua kisayansi mambo bila kutoonyesha hisia za wasomaji. Anatakiwa asiwe na majivuno na aheshimu anaowahakiki na anaowataka wasome uhakiki wake. Awachukue hatua kwa hatua kifalsafa hata waone vigumu, na kwamba haiwezekani kupigana naye.

 MISINGI YA UHAKIKI WA KAZI ZA KIFASIHI

Uhakiki wa kazi za kifasihi hufanywa kwa kuzingatia vipengele vya fani na maudhui. Fani na maudhui ni kama masanduku makubwa ambayo mhakiki huyafungua na kuanza kuchunguza vilivyomo ndani yake. Kila moja lina vipengele vidogovidogo ndani yake.

(a)Fani

Fani ni mbinu au ufundi anaobuni na kutumia mtunzi wa kazi ya kifasihi ili kufikisha ujumbe  kwa hadhira yake iliyokusudia. Fani ina vipengele mbalimbali. Vipengele hivyo ni pamoja na wahusika, mandhari, lugha, muundo na mtindo.

1)Wahusika

Wahusika wa kazi ya kifasihi ni viumbehai au wasio hai; halisi au wa kubuni, ambao wanatenda matendo mbalimbali ndani ya kazi ya kifasihi. Wahusika wanaweza kuwa ni binadamu, mawe, miti, malaika, miungu na mizimwi. Kwa kawaida, wahusika katika kazi ya kifasihi hutumika kuwakilisha au kubainisha maisha halisi ya wanadamu.

Aina za wahusika

Wanafasihi mbalimbali wamewagawa wahusika katika makundi tofauti. Hata hivyo, sisi tutawagawa katika makundi makuu mawili, yaani wahusika wakuu na wahusika wadogo.

·       Wahusika wakuu

Mhusika mkuu ni mhimili wa kazi ya kifasihi na huonekana kuanzia mwanzo hadi mwisho wa kazi ya kifasihi. Mhusika mkuu ndiye wa muhimu kabisa kuliko wote. Huyu ndiye anayehusiana zaidi na dhamira kuu ya kazi inayohusika.

·       Wahusika wadogo

Hawa ni wahusika wanaomsaidia mhusika mkuu kufikisha ujumbe wa mtunzi kwa hadhira. Kwa kawaida, wahusika wadogo huchomoza hapa na pale kwenye kazi ya kifasihi, kisha huweza kutoweka kwa muda au kutoweka kabisa. Kwa mfano, mhusika mdogo masikini anaweza kupambanishwa na mhusika mkuu ili kubainisha ukarimu au uchoyo wa mhusika mkuu, kisha huyo mhusika mdogo hatumwoni tena. Wahusika, wawe wakubwa au wadogo, wanaweza kuwa duara, bapa au shinda:

§  Wahusika duara

Wahusika duara (au mviringo) ni wahusika wenye sifa halisi za ubinadamu, yaani wanaonekana ni binadamu halisi. Hii ni kwa sababu wanabainisha katika maisha yao uzuri na ubaya – wema na uovu, ujasiri na woga, ushindi na kushindwa. Pia, wanabadilika kiakili, kimtazamo na kimaadili kadiri wanavyokutana na changamoto za kimaisha kama ilivyo kwa binadamu halisi.

§  Wahusika bapa

Hawa ni wahusika ambao hutokea wakiwa na tabia ya aina moja kuanzia mwanzo hadi mwisho.Wao hawakui au kubadilika,bali hubakia na msimamo au mtazamo ule ule walioanza nao. Kama ni mchoyo, anakuwa ni mchoyo kuanzia mwanzo hadi mwisho.

§  Wahusika shinda

Hawa ni wahusika ambao wako katikati ya wahusika duara na bapa. Wahusika hawa wanaweza kubadilika, lakini si kutokana na misimamo yao, bali ni kwa sababu ya kuyumbiswa na wahusika wengine. Ni wahusika ambao hawajitegemei kimawazo.

Tunaweza kuonyesha aina za wahusika kwenye mchoro kama ifuatavyo:

Wahusika

 

Duara

Shinda

Bapa

Wadogo

Wakuu

Shinda

Duara

Bapa

 











2.   Mandhari

Mandhari ni mahali ambako matukio ya kwenye kazi ya kifasihi yanatokea.Mandhari yanaweza kuwa halisi au ya kubuni tu. Kwa mfano, mtunzi anaweza akawaweka wahusika wake kwenye Jiji la Dar es Salaam. Haya ni mandhari halisi. Vilevile, anaweza kuwaweka wahusika kwenye nchi iliyoko chini ya bahari au kwenye jua. Hayo yanakuwa si mandhari halisi bali ni ya kufikirika  au ya kubuni tu.Kwa hiyo, mandhari yanaweza yakawa mjini au kijijini, msituni au baharini, chini ya ardhi au angani.

3 .Lugha

Lugha ndiyo malighafi kuu inayotumiwa na mtunzi kuzalisha kazi ya kifasihi. Lugha ya kifasihi ni lugha yenye mvuto kwa vile husheheni maneno ambayo yameshibishwa taswira au picha, yaani ni lugha ya picha.Lugha ya kifasihi ni ya picha kwa kuwa ina mambo yafuatayo:

(a)       Nahau

       Haya ni maneno, aghalabu mawili au zaidi, ambayo maana yake ya jumla ni tofauti na maana ya neno mojamoja ndani ya nahau hiyo. Kwa mfano, kuvunjika kwa moyo si kitendo cha moyo ulio ndani ya mwili kukatika vipande, bali nikukata tama.Nahau hunogesha na kunakshi lugha, hivyo huongeza mvuto na kuupa uzito ujumbe uliokusudiwa.

             (b)Methali

Huu ni usemi mfupi wa hekima ambao kwa kawaida huwa umerithiwa kutoka vizazi vya nyuma, na ambao umebeba maana pana iliyojificha. Kwa mfano, kidole kimoja hakivunji chawa.

                (c)Tamathali za semi

Hii ni misemo ambayo hutumiwa kutoa maana tofauti na maana ya maneno yake. Zipo aina mbalimbali za tamathali za semi. Zifuatazo ni baadhi yake:

Ø Tashibiha

Huu ni ulinganishaji wa vitu au hali mbili tofauti kwa kutumia maneno: kama, mithili ya, sawa na, utadhani na, mfano wa.Kwa mfano:

·       Ametuliakama gogo la mnazi.

·       Tumbo limetanguliamithili yangoma ya gwaride.

·       Ana macho makaliutadhanimatone ya gongo.

Ø Sitiari

Huu ni ulinganishaji wa vitu au hali mbili moja kwa moja bila kutumia maneno: kama, mithili ya, utadhani na mfano wa.

                Kwa mfano:

·       Kichwa chake ni benki ya majina ya shule nzima.

·       Maji ya kifuu ni bahari ya chungu.

·       Huyu mtoto atakuwa kiboko ya wote.

Ø Mubalagha

Huu ni uelezaji wa jambo kwa kutia  chumvi kuliko hali halisi ilivyo.

                Kwa mfano:

·       Yaani Yule ana tumbo kama gunia.

·       Huyu dada anaweza kuongea hadi simu ikaishiwa chaji.

·       Kwa njaa niliyo nayo, naweza kumaliza hata mbuzi wawili.

Ø Tashihisi

Hii ni njia ya kuvipa vitu visivyo binadamu sifa za ubinadamu, kwa mfano sifa za kuongea, kufikiri, kucheka na kutoa hoja.

                Kwa mfano:

·       Jua lilitudokolea jicho lake kali na kututemea moto wake hadi tukaenda kujificha chini ya dari.

·       Homa ile ilimng’ang’ania kwa makucha yake huku ikimvutia gizani,lakini alipambana nayo hadi ikatimua mbio.

·       Mlango ule ulitukaribisha kwenye tumbo la nyumba ile huku madirisha yakitukodolea macho kwa mshangao.

Ø Taashira

Hii ni njia ya kutaja kitu fulani  kwa lengo la kuwakilisha kitu au jambo jingine.

                    Kwa mfano:

·       Mwanafunzi Yule si kama wengine. Yeye amewekakitabu mbele.(Kitabu kinawakilisha masomo.)

·       Ni vema kwa kuwa ameamua kuishi maisha ya jembe.

(Jembe linamaanisha kilimo.)

Ø Taniaba

Hii ni njia ya kutumia jina fulani kwa namna ya ulinganisho ili kumaanisha kitu kingine. Hivyo viwili vinakuwa na tabia fulani linganifu.

                                                        Kwa mfano:

·       Kiongozi Yule amekuwa ni Iddi Amini wanchi ile.

·       Sisi tunafuga mbuzi tu. Hawa ndio ng’ombe wetu.

Ø Majazi

Hii ni aina ya tamathali ambayo hutaja sehemu tu ya kitu kwa lengo la kumaanisha kitu kizima.

                    Kwa mfano:

·       Masomo haya yanahitajivichwakwelikweli. (kichwa = mtu mwenye akili)

·       Ajali ile imepoteza roho saba. (roho = mtu kamili)

Ø Dhihaka

Haya ni maneno yenye maana kinyume na vile yanavyosema, ambayo hutolewa kwa lengo la kudunisha au kushusha hadhi.

                Kwa mfano:

·       Kijana huyu asione chakula; macho humtoka na miguu humwasha. Domo hujaa mate tele kama fisi aliyeona nyama.

·       Bosi wetu alikaa kwenye kiti chake, utadhani kakumbatia tungi la pombe ya kienyeji. Ama kwa hakika bosi kajaliwa tumbo. Tumbo hilo ni shimo refu ambamo zinaishia fedha za kampuni na jasho letu.

Ø Tasfida

Haya ni maneno ya heshima yanayotumika ili kupunguza ukali wa jambo linalosemwa, ambalo aghalabu, huwa aibu kulitamka mbele ya watu.

Kwa mfano:

·       Sehemu za siri                               

·       Amechafua hewa

·       Yuko uani

Ø Shtihizai,

Hii pia huitwa kejeli. Haya ni maneno ambayo yamekusudiwa kuleta maana kinyume na maana ya kawaida ya maneno hayo. Kwa mfano, kumwita mtu mweusi tiimzungu aucheupe; au mtu mwembamba sana kumwita bonge ni shtihizai au kejeli.

(i)             Ritifaa

Katika tamathali hii, mtu huzungumza na mtu au kitu ambacho hakipo pamoja naye kama kwamba yuko nacho.

                                                            Kwa mfano:

·       “Nyerere na Karume, mlitupenda wanenu; mkatuwekea misingi ya upendo na amani. Ona sasa wameingia mbweha na fisi ulingoni. Ninajua kabisa hamngekuwa radhi nao hata kwa dakika moja!”

                        Mbinu nyingine

Kuna mbinu nyingine za kifasihi ambazo msanii anaweza kuzitumia, ambazo si tamathali za semi. Mbinu hizo ni pamoja na:

Takiriri

Hii ni mbinu ya kurudiarudia manenokwa lengo la kusisitiza jambo.

                                                                      Kwa mfano:

·       Wewe utafungwa, utafungwa utafungwa tu!

·       Ukifika pale ni kula, dansi; kula, dansi!

·       Rudi mwanangu; mwanangu rudi; rudi tu mwanangu; nitakupokea.

Takriri, pia inaweza kuwa ni kurudia sauti ileile katika neno zaidi ya moja ambayo yanafuatana karibu karibu.

                                              Kwa mfano:

·       Matata alitamka maneno matano matamu. (sauti ma)

·       Sili wali ilhali ukali wa pilipili uko mbali. (sautili)

·       Alipanda kwenye kitanda akajitanda shuka lake. (sauti nda)

Tanakali sauti

Hii ni mbinu ya kuiga sauti fulani. Pia, hujulikana kamaonomatopea.

                                                                          Kwa mfano:

·      Kakachakakacha za kutembea kwao ziliniamsha usingizini.

·       Mara tulisikiango, ngo, ngo,mlangoni.

·       Kabla hatujakaa sawa, gari lile lilipita kama mshale,fyaaaa!

Tashtiti

Katika mbinu hii, msanii huuliza swali ambalo jibu lake liko wazi.

                Kwa mfano:

·       Kaka alipofika pale, alimwona rafiki yake akiondoka. “Unaenda kweli?” aliuliza kwa kutoamini.

·       “Ya nini kujisumbua? Ah! Acha nikalale zangu,” alijisemea Mawazo.

·       “Mara hii umesharudi?” Nilimuuliza kwa mshangao.

Mdokezo

Hii ni mbinu ya kuanzisha mazungumzo au wazo,kisha unaishia njiani bila kulimalizia. Hii ni kwa sababu,kwa namna fulani, sehemu ambayo haikumaliziwa inaeleweka kutokana na muktadha wa mazungumzo au maelezo yenyewe.

                      Kwa mfano:

                        Mama:     Yaani Doto, umevunja tena kikombe?

                                        Njoo hapa! Leo nitaku……..!

                        Doto:               Mama nisamehe. Bahati mbaya.

Mjalizo

Hii ni mbinu ya kupanga maneno katika mlolongo bila kuweka viunganishi kati yake.

                                     Kwa mfano:

·       Wewe lia, cheka, imba, lakini hutoki hapa!

·       Yule bwana alikaa chini, alisisimama, alijilaza chini, lakini maumivu yalibaki palepale.

·       Sisi tulifanya kila njia. Tuliita, wapi! Tukatafuta, wapi! Tukapiga simu, wapi! Mwishowe tukasema, liwalo na liwe!

Taswira

Utengenezaji wa taswira katika kazi za kifasihi ni mbinu inayojitegemea,bali huambatana na mbinu nyingine, kwa mfano, tamadhali za semi. Taswira ni picha zinazoumbika akilini ambazo tunazipokea kana kwamba ni kupitia kwenye milango ya fahamu.

                               Kwa mfano:

·       UKIMWI unabugia watu katika domo lake na kuwatafuna bila huruma.

                          Ifuatayo ni mifano ya taswira mbalimbali:

Taswira za kuona

Kwa mfano:

·       Ana tumbo kubwa kama mtungi.

·       Uso wake umetokeza mbele utadhani wa tumbiri.

·       Nyumba ile ilikuwa kama kilima kikubwa chenye mapango ndani yake.

Taswira za kusikia

Kwa mfano:

·       Kicheko chake ni kama radi

·       Kelele za watu ukumbini zilikuwa kama maporomoko ya maji mengi.

·       Njaa husababisha tumbo langu kunguruma kama pikipiki.

·       Taswira za mguso

Kwa mfano:

·       Mikono ilikuwa inaparua kama msasa.

·       Alikuwa na ngozi nyororo  kama kikombe cha udongo.

·       Maneno yake yanachoma kama misumari ya moto.

             Taswira za kunusa

Kwa mfano:

·      Ungemhurumia kwa vile ambavyo mguu ule ulitoa harufu kama mzoga wa paka.

·       Huyo bwana usimkaribie aongeapo ni kama unachungulia kwenye debe la pombe ya mnazi.

                   Taswira ya kuonja

Kwa mfano:

·       Mwonekano wake ulileta uchachu ndani ya akili yangu.

·       Ana maneno makali kama pilipili.

 4. Muundo

Ni mpangilio na mtiririko wa kazi hiyo kwa upande wa visa na matukio. Hapa tunachunguza jinsi msanii wa kazi ya fasihi alivyofuma, alivyounda na alivyounganisha tukio moja na jingine, kitendo kimoja na kingine, wazo na wazo, sura moja na nyingine, ubeti na ubeti, hata mstari wa ubeti na mwingine.

        Aina za miundo

(a)          Muundo wa msago,huu ni muundo wa moja kwa moja ambao tunafatilia matukio mbalimbali tangu la kwanza hadi la mwisho kwa mbinu ya utelezi. Kwa mfano, mhusika huzaliwa, hukua, huchumbia au kuchumbiwa, huoa au kuolewa, huzaa watoto, huzeeka, hufa. Riwaya ya kuli (1978) imetumia muundo huu. Katika riwaya hii tunamwona Rashidi akizaliwa, akikua, anaanza kazi, anaoa, anaanza harakati za kudai haki za makuli na mwisho anafungwa.

(b)          Muundo wa kioo,huu ni muundo wa kimchangamano utumiayo mbinu ambayo huweza ama kumrudisha nyuma msomaji wa kazi aya fasihi katika mpangilio wa matukio yake au kuipeleka mbele hadhira ya kazi hiyo. Riwaya yaZaka la Damu(1976)  imetumia muundo huu.

(c)           Muundo wa rukia,huu ni muundo ambao visa hupandana. Katika muundo huu kunakuwa na visa viwili ambavyo hupandana katika kusimuliwa kwake, na mwisho visa hivi huungana na kujenga kisa kimoja. Mfano ni riwaya ya Njama(1981).

Katika ushairi muundo tunaangalia idadi ya mistari katika kila ubeti wa shairi. Kuna miundo ya aina mbalimbali:

(i)             Muundo wa Tathnia – kila ubeti wa shairi unakuwa na mistari miwili.

(ii)         Muundo wa Tathlitha – kila ubeti unakuwa na mistari mitatu.

(iii)      Muundo wa Tarbia – kila ubeti unakuwa mistari minne.

(iv)       Muundo wa Takhimisa – kila ubeti unakuwa na mistari mitano.

(v)          Muundo wa Sabilia – kila ubeti unakuwa na mistari sita na kuendelea.

5.   Mtindo,ni ile namna ambayo msanii hutunga kazi hiyo na kuipa sura ambayo kifani na maudhui huainisha kanuni au kaida zilizofuatwa kama ni zilizopo au ni za kipekee.Mtindo ni upangaji wa fani na maudhui katika kazi ya fasihi kwa njia ambayo hatimaye hutokeza au huonyesha nafsi na labda upekee wa mtungaji wa kazi hiyo.

Dhima ya mtindo

-        Humwezesha msomaji kujua hisia za msanii kuhusu analiandika.

-        Humsaidia msomaji kutafiti thamani ya maudhui na namna ya kuyapima au kuyathamini.

-        Hudokeza kiasi cha hisia na mwamko wa wahusika katika hadithi, na vilevile kuonyesha maendeleo yake.

-        Ni kiungo muhimu cha mtiririko wa matukio.

-        Huiumbua dunia ulimwengu wake ambapo yale maono ni ya msanii, lakini mtindo ndiyo unaojitokeza kwa watu wengi ili wajue msanii anaandika kitu gani.

Katika mtindo kinachotazamwa ni:Matumizi ya lugha,Nafsi alizotumia msanii,Matumizi ya monolojia (maelezo), masimulizi na dialojia (mahojiano)

(b) Maudhui

Maudhui katika kazi ya fasihi ni jumla ya mawazo yanayozungumzwa pamoja na mtazamo wa mwandishi juu ya mawazo hayo. Maudhui hujumuisha mawazo pamoja na mafunzo mbalimbali yaliyomsukuma msanii hadi akatunga na kusaka kazi fulani ya fasihi.

Vipengele vya maudhui

·       Dhamira,Hii ni wazo kuu au mawazo mbalimbali yanayojitokeza katika kazi ya fasihi. Dhamira hutokana na jamii. Kwa kawaida dhamira huweza kuwa za kisiasa, kiutamaduni au kiuchumi. Katika dhamira, kuna dhamira na dhamira ndogondogo.

·       Mtazamo,ni hali ya kuyaona mambo katika maisha kwa kuzingatia mazingira aliyonayo msanii mwenyewe. Wasanii wana mitazamo ya aina mbili:

-        Mtazamo kiyakinifu– Huutazama ulimwengu au mazingira yanayomzunguka binadamu na mfumo wa kihistoria. Mtazamo huu humfanya msanii kuutazama ulimwengu kama kitu dhahiri katika uhalisi wake.

-        Mtazamo wa kidhanifu – Huu huchukulia ulimwengu kama kitu kinachobadilika kulingana na matakwa ya Mungu. Msanii mwenye mtazamo huu, atawasilisha hivyo katika kazi yake.

·       Msimamo,hii ni hali ya mwandishi kuamua kufuata na kushikilia jambo fulani.Jambo hili linaweza kuwa halikubaliki na wengi,lakini yeye atalishikilia tu. Msimamo wa msanii ndiyo unaosababisha kazi ya sanaa iwe na mwelekeo maalumu na hata kutofautiana na kazi za wasanii wengine.

·       Falsafa,huu ni mwelekeo wa imani ya msanii. Msanii anaweza kuamini, kuwa mfano, mwanamke si chombo duni kama wengine wanavyoamini. Au, kwa wale wapinga usawa, wanaweza kuwa na falsafa ya kumwona mwanamke kuwa kiumbe duni.

Kwa hiyo, falsafa ya kazi ya fasihi inatakiwa ichambuliwe kwa kuzingatia jinsi kazi hiyo ilivyoutazama ulimwengu na kuueleza ukweli juu ya mambo mbalimbali. Ukweli huo lazima uhusishwe na binadamu.

·       Ujumbe na maadili

Ujumbe katika kazi ya fasihi ni mafunzo mbalimbali ambayo hupatikana baada ya kusoma kazi ya fasihi.

·       Migogoro

Migogoro ni mivutano na misuguano mbalimbali katika kazi ya fasihi. Katika migogoro kuna migogoro kati ya wahusika ama vikundi vya wahusika, familia zao, matabaka yao, n.k. Na migogoro hii mara nyingi hujikita katika uhusiano wa kijamii. Migogoro yaweza kuwa ya:Kuichumi,Kiutamaduni,Kisiasa,Kinafsia

MADA NDOGO-2; MAENDELEO YA FASIHI

  CHIMBUKO LA FASIHI NA SANAA.

Kuna mitizamo mikuu minne  ya kiulimwengu inavyotokeza katika suala la chimbuko la fasihi .Mitazamo hiyo ni  kama ifuatayo;

1.   Mtazamo wa kidhanifu.

Mtazamo wa kidhanifu wa misingi yake katika kudhani tu kwa hiyo kufuatana na mtazamo huu inaaminika kuwa fasihi na Sanaa kwa ujumla kutoka kwa Mungu kwa hiyo mwanasanaa huipokea ikiwa imekwishapikwa na kuivishwa na Mungu huyo.

Mtazamo wa namna hii ulijitokeza tangu zamani sana wakati wanafalsafa wa mwanzo wa kigiriki na kinenzi kama vile Socrates Plato na Anstotle,walipoanza kuingia katika ulimwengu wa nadharia ya Sanaa. katika uwanja wa nadharia ya fasihi/Sanaa ya Kiswahili kuna mifano mingi ya wahakiki wa mwanzo waliokuwa na mitazamo sawa naya wanafalsafa hao mfano F.Nkwera (1970),  insha yake ya fasihi inadhihirisha uaminifu wake wa mawazo ya kidhanifu kwa kudai “fasihi ni Sanaa ambayo huanzia kwa muumba humfikia mtu katika vipengele mbalimbali -ni hekima ambayo mtu ameshirikishwa apate kumtambua muumba  wake”.Nkwera ameungwa mkono na wahakiki wengine ambao wanasisitiza mtazamo huu kwa kusema“Mtengenezo ya Sanaa huonekana kuwa ni shughuli ya kiungu yenyekumwiga Mungu ambaye ndiye msanii wa kwanza”

John Ramadhani pia katika makala yake ya fasihi ya Kiswahili anasisitiza kuwa.“Zaidi ya kwamba fasihi ni hisia vile vile kitengo cha mtu cha kubaini kazi ya Sanaa ni uigaji wa Mungu ambaye ndiye mfalme wa Sanaa zote”.Mawazo haya ya akina Nkwera,John Ramadhani na wengine yamejaa   mwangwi tu wa mawazo yaliyochakaa ambayo yalikwisha kutajwa na kushughulikiwa  na wahakiki wa zamani tuliowataja kwa msimamo huu wa kidhanifu,Sanaa au fasihi havijifinyangwi kwa jitihada za akili za mikono ya mtu   bali hupokelewa kutoka katika mikono mbayo mtu hana uwezo wa kuiona.

Udhaifu, mtazamo  huu  umepotosha maana halisi kwa kuchanganya Imani na taaluma,pia unajaribu kumtenganisha msanii na jamii yake kwani unatoa nadharia inayomwinua msanii na kufanya aonekane kuwa  mtu wa ajabu aliyekaribu na Mungu kuliko watu wengine wa kawaida.

2.   Mtazamo wa kiyakinifu

Kulingana na mtazamo huu Chanzo cha fasihi  ni sawa na chanzo cha binadamu wenyewe yaani Binadamu na mazingira yake ndio Alfa na Omega ya fasihi.Iwe kwa kuumbwa au mabadiliko kuanzia chembe hai ambayo imepitia maendeleo kadha ya makuzi hata kufikia mtu binadamu alioanishwa na kazi ili kuyabadili mazingira yake.Katika harakati zake za kujiendeleza kiuchumi kila mara alijaribu hiki na kile alichokiona kinafaa alikiendeleza Zaidi na kukidumisha katika hali hii hadithi(ngano),methali,vitendawili,nyimbo,tenzi(mashairi) n.k vyote hivyo vilitungwa na kusimuliwa kwa madhumuni  ya kufunza,kukosoa,kuadhibu,kuchokoza fikra na kuliwaza jamii baada ya kazi.

Sanaa hii ilirithishwa toka kizazi hadi kizazi kwa njia ya masimulizi na binadamu alivyozidi kujiendeleza kisayansi na kiteknolojia akahifadhi taaluma hii katika maandishi.Ndiyo sababu tunasema chanzo cha fasihi ni sawa na chanzo cha binadamu mwenyewe na jinsi binadamu alivyozidi na atakavyozidi ndiyo taaluma hii ilivyokuwa na kuendelea.

3.   Fasihi inatokana na sihiri,Istilahi Sihiri’ ina maana ya Uwezo au nguvu ya kimiujiza inayotumiwa na watu kusababisha matokeo fulani.Watalaam  hawa wanadai kuwa  chimbuko la fasihi ni haja ya mwanadamu kukabiliana na  kujaribu kuyathibiti mazingira yake. Haja hiyo haikutimilika ipasavyo katika hatua zake za mwanzo  za maendeleo ya mwanadamu kwani uwezo wa kisayansi na kiteknolojia wa mwanadamu wa wakati huo bado ulikuwa kiwango cha chini sana.Hivyo Imani au miujiza ilichukua nafasi ya sayansi na ugunduzi.Fasihi ilichimbuka kama chombo cha sihiri  hivyo katika kujaribu kuyashinda mazingira,Mfano Wawindaji walichora picha ya mnyama waliyetaka kumuwinda kabla ya kwenda kuwinda,kisha walichoma mkuki au mshale kwa kuamini kuwa kitendo hicho kitatokea kuwa kweli watakapo kwenda kuwinda. Nyimbo walizoimba wakati wa kufanya sihiri hiyo ndiyo fasihi ya mwanzo.

Udhaifu wa nadharia hiini kwamba inachangnya dhima na chimbuko kwani kutumika kwa nyimbo au ushairi katika sihiri hakuthibitishi kuwa sihiri ndiyo chimbuko lake.Sihiri ni amali moja tu kati ya amali nyingi za wanadamu wa mwanzo zilizotumia ushairi.

4.   Nadharia ya Mwigo,Wataalam wa nadharia wanadai kuwa Fasihi imetokana na mwigo(Uigaji),Katika nadharia hii inaeleza kuwa mwanadamu alianza kuwa mbunifu kwa kuiga maumbile yaliyomzunguka.Hivyo sanaa za mwanzo mara nyingi zilijaribu kusawiri vitu vilivyomo katika mazingira ,mfano wanyama,ndege,miti,watu.Nadharia hii ni kale,ilianzisha na wataalamu wa kiyunani  na walioieneza zaidi niPlato (Republic) na Aristotle (Poetics)  Platoanahusisha mwigo na dhana ya uungu.Anaeleza kuwa Maumbile na vilivyomo ni mwigo tu wa sanaa ya kiungu.Sanaa ya Mwanadamu (Hususani ushairi) ambayo huiga tu mambo hayo yaliyomo  katika maumbile haiwezi kuwa na ukweli  au uhalisi wa kuwa inaiga maumbile ambayo na yenyewe  yanaiga kazi ya Mungu.Hivyo alishauri aina fulani za ushairi zipigwe marufuku kwa sababu zinapotosha ukweli.

   Udhaifu wa nadharia hii ni kwamba inasisitiza mno uigaji na kusahau suala la ubunifu katika sanaa na fasihi.Kama wasanii wangeig maisha na mazingira tu,sanaa yao ingepwaya sana na haingekuwa tofauti na picha ya fotografia au maelezo ya matendo ya mazingira na matendo ya kila siku ya mwanadamu.

FASIHI NI SANAA.

Sanaa ni uzuri unajitokeza katika umbo lililosanifiwa umbo ambalo mtu hulitumia kuelezea hisia zinazomgusa kwa kutoa kielelezo au vielelezo vyenye maana maalumu.

Aina za Sanaa

Ø Sanaa za Uonyeshi,ni sanaa ambazo uzuri wake hujitokeza katika umbo la kudumu, umbo ambalo linaweza kuhifadhiwa na uzuri wake kuonyeshwa wakati wowote. mfano uchoraji, uchongaji, kutarizi, ufinyanzi, n.k. Sanaa ambazo hututolea vitu kama vile picha, vinyago, nguo zilizotarizwa, vyungu n.k.

Ø Sanaa za Ghibu,ni sanaa ambazo uzuri wake haujitokezi kwenye umbo linaloonekana kwa macho au kushikika bali  katika umbo linalogusa hisia mfano ushairi, uimbaji, upgaji muziki, n.k. Uzuri wa sanaa hizi umo katika kuzisikia.

Ø Sanaa za Vitendo,ni sanaa ambazo uzuri wake umo katika umbo la vitendo. Uzuri wa sanaa  hizi umo katika umbo la vitendo, na ili kuupata uzuri huu yampasa mtu kutazama vitendo vikifanyika. Umbo hili linalazimisha kuwepo kwa mwanasanaa (mtendaji) na mtazamaji(Hadhira) wa sanaa mahali pamoja kwa wakati mmoja, ama sivyo sanaa haikamiliki. Hali hii ndiyo inayosababisha sanaa hizi za vitendo kuita sanaa za maonyesho kwa sababu lazima wakati zinapototendeka awepo mtu wa kuonyeshwa, maana uzuri wake umo katika vitendo vyenyewe.

SIFA ZA SANAA ZA MAONESHO

-         Dhana ya kutendeka (tendo)

-         Mtendaji (fanani)

-         Uwanja wa kutendea/jukwaa maalumu

-         Watazamaji (hadhira).

Hivyo sanaa za maonyesho ni dhana zilizo kwenye umbo linalotendeka na  ili dhana hii itendeke inahitaji mtu wa kuitenda (mtendaji). Mtendaji huhitaji uwanja wa kutendea hiyo dhana, na wakati akiitenda hiyo dhana wanakuwepo watazamaji.

 Tanzu za Sanaa za Maonyesho

1)Tambiko, ni sadaka inayotolewa kwa miungu au mahoka, mizimu, pepo, n.k.  wakati wa kusalia miungu.Matambiko yalikuwa na umuhimu mkubwa katika jamii za babu zetu kuliko siku hizi. Jamii ya asili ilipokabiliwa na matatizo yaliyowashinda kama vile magonjwa, ukame, au kukosa mtoto, n.k. walifanya tambiko na kusali ili miungu yao iwasaidie. Wakati fulani walifanya matambiko kwa ajili ya kuomba radhi au kutoa heshima na shukrani.

Mara nyingi matambiko haya huandamana na kafara kama sadaka inayotolewa na jamii kwa wahenga wao. Kafara inaweza kuwa ya kuku, kondoo, ng’ombe, mbuzi au chakula. Katika jamii nyingi za Kiafrika kabla ya ukoloni walitoa kafara ya binadamu.

 Fani katika tambiko

Ø Sanaa

Katika tambiko sanaa inayotendeka ni ule ufundi wa kutenda vitendo kwa ukamilifu kwa kutambika kwa kutumia ufundi wa aina fulani.

Ø Wahusika

Wahusika wa tambiko ni wale wazee maarufu walioteuliwa na jamii kuendesha shughuli hizi za matambiko. Si watu wote katika jamii huhusika.

Ø Mazingira (Mahali)

Tambiko linaweza kufanyika porini, makaburini, njia panda, kwenye mti mkubwa au mahali popote kutegemeana na aina ya tambiko lenyewe.

Umuhimu wa Tambiko

ü Hujenga imani kama chombo cha kutatulia matatizo ya jamii. Jamii ya asili ilipokabiliwa na matatizo ilifanya tambiko na kusali ili miungu iwasaidie kuondokana na tatizo hilo.

ü Tambiko husaidia kuendeleza mila na desturi za jamii.

ü Tambiko hujenga na kuimarisha mahusiano miongoni mwa wanajamii.

ü Matambiko huiongoza jamii katika mapambano dhidi ya matatizo mbalimbali yanayowakabili.

Hasara za Tambiko

ü Hujenga dhana potofu katika jamii kwani watu huamini nguvu fulani bila kuwa na uhakika au uthibitisho wa kisayansi.

ü Huleta hasara kubwa kwa jamii kwani kafara ya tambiko inahitaji mnyama au chakula, ambapo watu hutumia hela nyingi kuvipata vitu hivyo.

2) Mivigha,ni sherehe zinazofanywa na jamii katika kipindi maalumu cha mwaka. Mivigha hufanywa  kwa lengo la kufundisha jambo fulani maalumu kwa maisha ya jamii. Sanaa za maonyesho katika kundi hili zinahusu kuingizwa kwa mwanajamii kwenye kundi la watu wa aina fulani kutoka kundi la watu wa aina nyingine. Mfano jando na unyago, harusi, kutawazwa chifu, n.k.Katika jando na unyago mtu hutoka kundi la watoto kuingia kundi la watu wazima, mtu aliyeoa anatoka kundi la makapera kwenda kundi la waliooa au kutawazwa chifu, mtu anatoka kundi la raia na kuingia kundi la watawala n.k.

Kutoka kundi moja kuingia kundi jingine ni hatua iliyopewa umuhimu mkubwa katika jamii ya asili. Umuhimu huu uliambatana na madaraka mapya yaliyo mkabili mwanajamii kuingia katika kundi jipya. Kila kundi la watu lilikuwa na madaraka fulani mbayo kutekelezwa kwake ndiko kulikoleta maendeleo ya jamii .

   Fani katika  Mivigha

Ø Sanaa

Sanaa katika mivigha ni ule ufundi wa kutenda kikamlifu na kiufundi katika kudhihirisha yale yanayotendeka.

Ø Wahusika,Katika mivigha wahusika ni wa aina tatu:

a)Mtendaji/watendaji,ni wale wote wanaoshiriki kutenda ile dhana ya kuwatoa watu kutoka kundi moja na kuwaingiza katika kundi lingine. Vitendo hivyo huambatana na nyimbo, michezo mbalimbali n.k.

b)Watazamaji ,ni wale wanaoingia kutoka kundi moja na kwenda kundi lingine. Hawa ndio watazamaji, kwa sababu maneno, nyimbo, vitendo, ngoma, n.k. vyote vinafanyika ili wao wavione na wajifunze na baadae watekeleze yale waliyojifunza.

c)Waangaliaji, ni wale wanaoangalia mambo yanayotendeka bila wao kushiriki katika kucheza au kuimba au kutoa mafunzo, wanaangalia tu. Hawa kwa upande wa sanaa za maonyesho sio watazamaji kwa sababu yale yafanywayo hayawasilishwi kwao. Wakiwepo au wasiwepo bado vitendo vinatendeka tu bila maana yake kupotea. Hawa wanaitwa “waangaliaji”

d)Mahali /Mandhari,kwa upande wa mivigha uwanja wa kutendea ni mahali sherehe zinapofanyika. Inaweza ikawa ndani ya nyumba, au porini, kwenye uwanja wa nje ya nyumba,milimani au mapanngoni, n.k.

Umuhimu wa mivigha

ü Mivigha hufundisha umuhimu wa kazi kama vile kilimo, uwindaji, uhunzi, ufinyanzi, ushonaji, n.k.

ü Mivigha huhimiza umuhimu wa ujasiri katika maisha.

ü Mivigha  hufundisha suala zima la unyumba na malezi kwa ujumla mfano  umuhimu wa uzazi na malezi bora.

ü Mivigha husisitiza umuhimu wa umoja na ushirikiano katika jamii.

          Hasara za Mivigha

ü Hugharimu pesa nyingi sana ambapo huwaacha wenye sherehe kwenye madeni makubwa.

ü Sherehe huweza kusababisha ugomvi, chuki, dharau, tamaa, n.k.

ü Huleta ushindani na matokeo yake husababisha baadhi ya watu wasio na uwezo hujiingiza katika wizi, utapeli, ujambazi, n.k.

  3. Majigambo, ni masimulizi ya kujigamba kwa mtu kuhusu mambo ya kishujaa aliyopata kuyatenda maishani mwake. Majigambo hayo husimuliwa katika lugha ya kishairi na masimulizi yake huambatanishwa na vitendo vya mjigambaji mwenyewe.

Mtambaji anapotamba katika sanaa hii, kwa kawaida huwa na tabia ya kujivuna au kujitapa kuwa yeye ni bora kuliko wengine wote.Wakati wa utambaji mazingira humtawala fanani. Pengine fanani alikuwa akitamba kuonyesha utukufu wake kwa mfalme wao. Au alikuwa akitamba wakati wa kujiandaa kwenda vitani.

Fani katika Majigambo

Ø Sanaa

Sanaa katika majigambo ni ule ufundi anaoutenda mjigambaji, kwa kujigamba kwa ufundi huku akionyesha vitendo waziwazi alivyopata kuvitenda maishani mwake.

Ø Wahusika

Hapa kuna mtendaji na watazamaji

·       Mtendaji,ni yule anayejigamba mbele ya wenzake, yaani Yule anayejigamba kuhusu mambo yake ya kishujaa aliyoyatenda maishani mwake.

·      Watazamaji,ni wale wanaotazama vitendo vinavyotendwa na mtendaji.

ØMahali/Jukwaa maalum

Uwanja wa kutendea ni mahali popote ambapo majigambo yanaweza kufanyikia. Hapa inaweza kuwa kwenye uwanja mkubwa ambapo sherehe hizo zinafanyikia au kwenye ukumbi.

Ø Matumizi ya Ngoma katika Majigambo

Majigambo vile vile yaliambatana na ngoma, wakati mwingine ngoma zilichezwa na katikati ya ngoma mjigambaji mmoja alijitokeza na kuanza kujigamba, alipomaliza alirudi kucheza ngoma na mwingine alijitokeza tena

   Umuhimu wa Majigambo

ü Hudumisha utu wa mwanaume katika jamii.

ü Hudumisha ari ya kuwa wakakamavu, shujaa na jasiri katika jamii.

ü Huburudisha jamii yaani mtendaji na wasikilizaji.

Hasara za Majigambo

ü Hukuza na kuendeleza ubinafsi kwani fanani huonekana ni bora zaidi kuliko watu wengine.

ü Mkusanyiko wa hadhira hutumia pesa au vyakula kwa wingi, hivyo husababisha umasikini .

ü Majigambo husababisha unafiki kwa sababu fanani huonyesha mafanikio yake tu na sehemu alizoshindwa hagusii kabisa, kitu ambacho si cha kweli katika maisha ya mwanadamu.

4.Michezo ya Watoto

Ni mchezo mbalimbali inayochezwa na watoto, na michezo hiyo hufungamana na hali ya utamaduni, uchumi na siasa ya jamii inayohusika. Mchezo hii husaidia watoto waweze kujifunza mambo mbalimbali yanayotokea katika jamii yao. Kwa njia hii watoto hujifunza shughuli mbalimbali za uzalishaji kama vile kilimo, kupika chakula, kuwinda, n.k. Vile vile hucheza mchezo wa baba na mama. Hapa mtoto mmoja anakuwa mama, mwingine baba na wengine watoto. Mchezo huu huakisi mambo halisi ya nyumbani.

   Fani katika Michezo ya Watoto

Ø Sanaa

Sanaa katika michezo ya watoto wadogo ni ule ufundi wa kutenda vitendo kikamilifu na kuonyesha ujuzi mkubwa katika utendaji huo

Ø Wahusika

Kuna watendaji na watazamaji. Watendaji ni watoto wenyewe wanaocheza michezo hiyo, yaani wavulana na wasichana. Idadi ya watendaji inategemea aina ya mchezo wenyewe.Watazamaji ni wale wanaotazama mchezo huo. Hapa  wanaweza wakawa watoto wenyewe ambao hawachezi au jamii inayowazunguka watoto hao.

Ø Mahali

Uwanja wa kutendea michezo ya watoto ni sehemu yoyote itakayochaguliwa na watoto wenyewe kulingana na michezo unaohusika. Kwa mfano, wanaweza kucheza uwanjani, chini ya mti, barabarani, chumbani, sebuleni, kando ya nyumba, n.k.

Umuhimu wa Michezo ya Watoto

·       Huwasaidia watoto wadogo kujifunza mambo mbalimbali yanayotokea katika jamii yao. Kwa njia hii watoto hujifunza shughuli mbalimbali za uzalishaji mali, utamaduni na siasa ya jamii yao.

·       Huwasaidia watoto kujifunza kuwa na ujasiri, ushujaa, udadisi wa mbinu mbalimbali za kupambana na matatizo yanayojitokeza katika jamii.

·        Hurithisha amali za jamii toka kizazi kimoja hadi kizazi kingine. Michezo hii hurithisha mila na desturi za jamii fulani kwa kucheza michezo hiyo.

·       Michezo hiyo huburudisha watoto. Katika kucheza michezo hiyo, watoto huburudika na kustarehe.

·       Huwasaidia watoto huimarisha viungo vya mwili kwa watoto wanaocheza michezo hiyo.

Hasara za Michezo ya Watoto Wadogo

·       Watoto huweza kuumizana kutokana na michezo hii.

·       Ikiwa wazazi wa watoto hawa wana tabia chafu kama ile ya kugombana, kutukanana ovyo, vivyo hivyo watoto hawa watarithi tabia chafu kutoka kwa wazazi wao na wanaweza kuwaambukiza wenzao.

5.   Utani, Ni hali ya kufanyiana mizaha pasipo kuogopa na kushtakiana au utani ni uhusiano wa kutaniana au kufanyiana masihara ambao ni tofauti na desturi za kutokuheshimiana. Madhumuni yake makubwa ni kupunguza na kuondoa kabisa uhasama na chuki iliyokuwepo baina ya makundi fulani ya watu.

Fani katika Utani

Ø Sanaa

Sanaa katika utani ni ule ufundi na uwezo wa kutaniana baina ya wahusika wanaohusika na utani huo.

Ø Wahusika

Katika utani, washiriki wanaweza kuwa mtu na mtu, familia na familia, kabila na kabila, ukoo na ukoo au nchi na nchi.

Ø Mahali

Uwanja wa kutendea inaweza kuwa mahali popote ambapo utani unaweza kufanyika. Inaweza ikawa kwenye harusi, msibani, kwenye pombe wakati watu wanakunywa, n.k.

Umuhimu wa Utani

·       Kutoa maadili na mafunzo fulani kwa jamii.

·       Kuimarisha umoja na ushirikiano miongoni mwa wanajamii (kujenga undugu)

·       Kuhimiza ujasiri na juhudi katika maisha.

·       Kuhimiza upendo katika maisha.

·       Hukuza na kuimarisha mila na desturi za jamii.

Hasara za Utani

·       Husababisha ugomvi katika jamii.

·       Huleta hasara za kuchukuliana vitu bila malipo.

·       Huvunja au kuvunjiana heshima miongoni mwa wahusika.

Muziki

Kazi za fasihi zipo katika nyanja zifuatazo uchoraji, ususi, fasihi, ufinyanzi, muziki, ufumaji, utarizi na maonesho.Nyanja hizi za Sanaa zinaweza kuonyeshwa kwenye kielelezo hiki:-

Ufumaji

Utarizi

                                         

Uchoraji

 

        Fasihi

     SANAA

                                                                                   

FASIHI                               

Ufinyanzi

                                                                                            

        Uchongaji

Maonyesho

Ususi

 



Kila kipengele cha Sanaa kinatofautiana   na kingine kwa umbo na matumizi. Fasihi ni kipengele cha Sanaa kinachotumia maneno kuumba huo uzuri wa kisanaa.

TOFAUTI KATI YA FASIHI NA TANZU NYINGINE ZA SANAA

1.   Lugha , kazi zote za kifasihi zinaundwa kisanaa kwa kutumia lugha inayotumika au kuandikika. Lugha hiyo hubeba maana Fulani (ujumbe) kwa jamii Fulani.Hivyo lugha ndiyo inayotufautisha fasihi na Sanaa nyingine. Kwa mfano, uchoraji kipengele chake muhimu kalamu, rangi na kipande cha nguo au karatasi. Ufinyanzi lugha yake ni udongo , uchongaji wa vinyago lugha yake ni gogo la mti n.k. Fasihi si maelezo ya kawaida kawaida kama vile matangazo, taarifa ya habari au barua, fasihi ni maelezo yenye mguso kisanaa. Kazi za kifasihi, huumbwa kimafumbo hutumia nahau au misemo , methali, tamathali za semi, taswira na ishara mbali mbali. Kazi za fasihi hufikirisha mtu huweza kutumia akili ili aweze kugundua kazi ya kifasihi aliyosoma au kuisikia kuwa ina maana gani.

2.   Wahusika,kazi yeyote ya fasihi inakuwa na wahusika wake ambao matukio mbali mbali yanayohusu jamii huwazungukia wahusika ni watu ama viumbe, waliokusudiwa wawakilishe tabia za watu katika kazi za fasihi. Kwa upande mwingine wahusika ni muhimu sana katika kutoa na kufikisha dhamira kwa hadira iliyokusudiwa na mwandishi.

3.   Mandhari, kazi ya fasihi inakuwa na mandhri ambayo huonyesha tukio linaponyika. Mandhari hiyo inaweza kuwa ya kubuni au ya kweli.Mandhari husaidia kujenga hisia inayokusudiwa na mwandishi.

4      . Utendaji, utendaji hasa katika fasihi simulizi hushirikisha fanani na hadhira kwa wakati mmoja. Vile vile utendaji humfanya fanani aweze kuonyesha baadhi yamatendo katika usimulizi wake.

5      Fani na maudhui,kazi za fasihi zina sehemu mbili yaani fani na maudhui na sehemu hizi zinafungamana. Maudhui ni kile kinachosemwa na fani ni namna kinavyosemwa. Kazi nyingine za Sanaa vile vile zinafanikisha ujumbe kwa hadhira lakini mbinu na vifaa vinavyotumika ni sehemu ya fasihi. Kwa ujumla kazi za kifasihi, fani na maudhui yake ni ya hali ya juu sana ukilinganisha  na Sanaa nyinginezo.

KWA VIPI FASIHI NI SANAA ?

    Usanaa wa fasihi hujitokeza katikavipengele mbali mbali kama ifuatavyo:-

1.   Mtindo, Sanaa katika fasihi hujidhihirisha katika namna kueleza jamii (mtindo) katika kueleza jambo kunakuwa na aina fulani ya kiufundi ambao mwanafasihi huutumia katika kufikisha ujumbe kwa jamii yake. Taarifa inayotolewa inaweza kufichwa katika fumbo, shairi, kitendawili, tamthiliya au hadithi.

2.   Muundo (mpangilio maalumu wa matukio),katika kazi ya fasihi, matukio yanapangwa kiufundi ili yaweze kuwasilishwa vizuri kwa jamii husika. Matukio hayapangwi ovyo ovyo tu bali yanakuwa na mpangilio maalumu.

3.   Utenzi mzuri wa lugha iliyojaa nahau, misemo, methali, tamathali za semi,taswira na ishara mbali mbali unaonyesha wazi usanaa wa fasihi. Lugha itumikayo katika fasihi ni ya kisanaa. Ni lugha iliyopambwa na inayokusudiwa kuibua hisia za namna Fulani kwa hadhira yake. Lugha hiyo inaweza kuchekesha, kukejeli, kubeza, kuchokoza, kutia hamasa au kushawishi. Matumizi ya lugha yako ya aina tofauti, kuna tamathali za semi, misemo, nahau, methali. Lugha ya wahusika hasa lahaja zao, uchaguzi wa msamiati,ufundi wa kutoa maelezo hasa ya wahusika ya mandhari na matukio, uteuzi wa lugha yenyewe itumiwayo.

4.   Uundaji wa wahusika, wahusika huwa na tabia zinazotofautiana kati yao. Wanaundwa kiufundi sana na msanii anaweza kuamua anataka wahusika wanaowakilisha tabia na matendo fulani tu katika jamii na kwa hiyo atawaumba wahusika hao ili kukamilisha nia na lengo lake.Katika kutofautisha tabia na hali za wahusika, mwandishi analazimika kutumia mbinu ya kuwapa majina wahusika wake. Wahusika wanaweza kuumbwa kinafsi au kiakili na kimwili. Kutokana na ujenzi wa aina hii mhusika huonyesha wasifu wake wa ndani na nje au anaweza kuonyesha mabadiliko yake kila anapokutana na mazingira tofauti.

5.   Ujengaji mzuri wa Mandhari, fasihi hujengwa katika mazingira maalum. Mandhari husaidia sana kujenga hisia inayokusudiwa na mwandishi. Mandhari yanajengwa kiufundi na mwandishi ili yasaidie katika kujenga kazi nzima ya fasihi.

FASIHI KAMA CHOMBO CHA UKOMBOZI

Ukombozi ni harakati za jamii yoyote zenye lengo la kuitoa jamii hiyo kwa nguvu (kwa silaha) au kwa mazungumzo kutoka katika makucha ya watumwa kisiasa,kiuchumi,kimawazo na kiutamaduni.Jamii inaweza kuwa ni ya kitumwa kisiasa ikiwa haitakuwa na fursa ya kushika hatamu ya uongozi wao na badala yake ikategemea uongozi kutoka kwa jamii nyingine jamii itaitwa ya kitumwa ,kiuchumi,ikiwa haitakuwa na haki ya kuendesha njia mbalimbali za uzalishaji mali.Pia jamii isiyoweza kufikiri na kuamua wala kutokuthamini mawazo yake yenyewe na badala yake ikawa katika mgawanyiko wa ibada na itikadi za kigeni ni jamii isiyo huru kimawazo vile vile jamii haitakuwa huru kiutamaduni ikiwa itakosa kuthamini uaminifu,uumbaji na ugunduzi wake yenyewe badala yake ikasujudu amali zilizo na chimbuko kutoka nje.Nyanja za ukombozi wa jinsi fasihi ya Kiswahili ilivyozitazama mpaka leo

(a)Kisiasa

Ukombozi wa kisiasa unapatikanaje?

Unapatikana tu baada ya kupigania uhuru wa bendera kuwa ndio wa kwanza kupatikana kwa nchi ambayo iko katika harakati za kujikomboa.Katika maandishi ya mengi fasihi ukweli huu unajitokeza kwa mfano katika utenzi wauhuru wa kenya msanii anatuonyesha  juu ya vita vya kumng’oa mkoloni kutoka katika kiti cha uongozi kwanza baada ya mwafrika kupandisha bendera yake mambo mengine yafuate vilevile katika utenzi wa uhuru wa Tanganyika na utenzi wa jamhuri ya Tanzania“mwandishi anasisitiza  uhuru wa bendera ukielezwa kuwa kabla ya ukombozi wa aina nyingine kufuata.

Kwa hiyo ukombozi huu wa mwanzo (uhuru wa bendera) husababisha uhuru wa kisiasa wanchi kisha uhuru wa kisiasa huwa ni jukwaa la ukombozi wa uchumi na mambo mengine,vitabu vingine vinavyozungumzia ukombozi wa kisiasa nimzalendo,F.E.MK Senkero) Ubeberu Utashindwa(J.K Kiimbila),Tone la Mwisho(E.Mbogo),Kinjikitile na Mashetani(E.Hussein),Nuru mpya(R.Rufeshobya)

(b)Kiuchumi

Uhuru wa bendera ni sehemu ya mwanzo tu wa ukombozi wa jamii nchi zinaweza kujidai ni huru kumbe uchumi wake bado ungali mikononi mwa nchi nyingine.Nchi nyingi zinazoendelea bado ziko katika harakati hii ya kutaka kujikomboa kiuchumi.Waandishi wengi wa fasihi ya Kiswahili  wamezungumzia sana suala la uchumi katika  mfano ‘’Mashairi ya Azimio la Arusha’’ mwandishi anaonyesha na kushambulia unyonyaji ambao ni adui wa uhuru wetu.

Vilevile waandishi wanasisitiza kufanya kazi kama njia ya kuimarisha uchumi.Pia wameeleza kuwa unyonyaji unaweza kukomeshwa kwa kutaifisha njia zote za uzalishaji mali na kuwa mikononi mwa umma. Pia Katika tamthiliya ya “Bwana Mkubwa” (J.P Mbonde) mwandishi ameonesha kuwa kwa sasa shabaha yetu sisi ni kupigana na ukoloni mambo leo ili kupata uhuru kamili.Ukoloni mambo leo ni kikwazo cha ukombozi wa kiuchumi. Kwa sababu ya ulegevu wa uhuru wa kisiasa nchi inaweza kuwa na mali  lakini ikizembea kufanya kweli ipasavyo yaweza kufanyiwa njama na ukoloni ndio maana upo umuhimu wa bidii katika kazi na uzalishaji wa mali kisha linafuata swala la ulinzi wa mali hiyo.

Kuzikomboa njia za uzalishaji mali hakutoshi kwani kila hila zao zisizoisha wakoloni wanaweza wakatupora mali hiyo tunapaswa kuwa macho.Katika utenzi wa “Zindiko la ujamaa” mwandishi anaeleza utaifishaji wa njia kuu za uchumi na uhalali wa utaifishaji huo. Mwandishi anaonyesha kuwa utaifishaji huo ulifanywa si kwa kuwaona wakoloni kuwa wanadhuluma bali kama njia moja wapo ambayo itaongeza kwenye ukombozi wa kiuchumi katika jamii. Lengo moja ni kufuta ubinafsi ambao unapelekea tofauti za kitabaka na badala yake manufaa ya umma kwa ujumla.

Ukombozi wa kiuchumi si utaifishaji wa njia za uzalishaji mali tu na wala si kukomesha ukabaila na ubepari bali ni kuongeza juhudi katika kazi mbali mbali ili kuongeza kiasi cha pato la kitaifa. Waandishi wengine wanazungumzia ukombozi wa kiuchumi ni kama vile, “Nuru mpya” (G. R. Ruteshubya) “Mashetani” (E. Hussein) “Sauti ya dhiki” (A. Abdallah) “Kasri ya mwinyi fuad” (Shafi Adam Shoji) Zetu bora mkulima na wasifu wa sili binti saad(S. Robert).

C) Kimawazo

Ukombozi wa kimawazo ni uhuru wa mtu katika upeo wa fikra pasipo kutegemea mtu mwingine. Hapa mtu aliye huru awe anajiamini mwenyewe na awe mtu kama watu wengine. Awe mwenye uwezo wa kuwaza, kuamua na kutenda, kuchanganua na kupanga kama watu wengine. Mtu aliye mtumwa wa kimawazo anaweza kufananishwa na mnyama wa kufugwa. Mnyama wa kufugwa daima ni mtumwa na bwana wake wakati wote huongojea amri kutoka kwa bwana wake.

Maandishi ya fasihi yanazungumziakwa upana swala hili la uhuru wa mawazo . Katika riwaya ya “Njozi za usiku” dhana hii ya utumwa wa kimawazo ipo ndani ya watu wengi ambao wanashikilia hasa baada ya maajilio ya elimu iliyokuja pamoja na ukoloni na ikatumika kwa upotofu. Katika riwaya hii msanii anaonyesha kuwa wale waliosoma walidharau kazi zote za mikono, walifikiri kuwa kazi za mikono zinafaa kwa wale ambao hawakusoma. Wao wanafikiri kuwa kazi ya mtu aliyesoma ni kushika kalamu na kuandika tu au kuwasimamia ambao hawakusoma.Tangu uhuru wa Tanzania kumekuwa na harakati za kufutilia mbal ukanganyifu wa namna hii katika mawazo ya watu. Mawazo ya namna hii ndio yamekuwa yakiwafanya watu wengi wa hali ya chini waamini kuwa uchumi walionao wamepewa na Mungu.

Vile vile kimawazo watu waliamini kwamba kila jambo lilitokana na watawala wa kizungu lilikuwa ni bora kabisa. Kwa mfano hata majina yliletwa toka Ulaya  nay a kwetu ya asili kuachwa. Haya yanajadiliwa wazi katika tamthiliya ya “Bwana mkubwa” (J. P. Mbonde)

Katika ukombozi wa kimawazo kuna swala la ukombozi wa mwanamke na swala la dini.Katika suala la ukombozi wa mwanamke watu wengi wanalitazama kirahisi jambo hili. Wengi wanadhani kuwa mwanamke hana haki ya kujibagua kutoka kwa wanaume na kujipigania haki yake. Watu hawa hawaelewi ni mapinduzi gani ambayo hawa wanapigania.Katika fasihi ya Kiswahili Shaban Robert amewatetea wanawake katika kazi zake mbali mbali ikiemo Diwani ya”Wasifu wa siti binti saad” na siku ya watenzi wote. Shaban Robert amemtazama mwanamke kama mtu anayestahili  utu kama watu wengine wowote wale.

Katika kitabu cha “Wasifu wa Siti binti Saad” msanii au mwandishi anaeleza wazi jinsi jamii ilivyomfanya mwanamke kama chombo cha kutunzwa utawani ili kiwe kizuri kipate kuwavutia wanaokitafuta na baada ya kutoka utawani kikawa mikononi mwa mwanaume kikamtegemea kwa hiyo mwanamke alikuwa ni mtu aliyechukuliwa kama hana wajibu wowote wa maana Zaidi ya kuwa mtegemeaji. Lakini Shabn Robert aliona kuwa ( uk 23) “Ukimdumisha mtu leo utamuona juu ya kilele cha utukufu kesho.

Mawazo ya mwandishi ni kwamba wanawake ni vyema watazamwe katika hali zao za maisha katika ubaya na uzuri kama wanaume. Kuhusu suala la dini linajitokeza katika riwaya ya “Kichwa maji”ambapo mwandishi anaona dini imeanzishwa na waoga ambao hutawaliwa na milango yao ya fahamu badalaya kutawaliwa na akili au bongo zao.

Jambo muhimu katika kumkomboa mtu kimawazo ni kwamba ikiwa dini itaendelea kuwepo isiwe na mtazamo duni na finyu na athari zake ambazo alikuja nazo mkoloni akidai kuwa tamaduni zetu ni za kishenzi. Sharti elimu ndiyo iwe ya kutafakari na kugeuza mfumo wa maisha ya jamii.

Katika dini pia kuna madhehebu mbali mbali ambayo kati yao kuna uhasama mkubwa, muislamu anadai kuwa yeye ni bora Zaidi kuliko mkristo na mkristo anajiona yeye ni bora kuliko muislamu. Madhehebu yote haya yamechimbuka huko mashariki ya kati…….katika kitabu cha “Bwana mkubwa” (uk 18-19”)……kwanini basi mlitutenganisha katika vikundi vidogo vya madhehebu tofauti kati ya wakristo na waislamu iwapo Mungu ni yule yule mmoja leo mnatueleza tuombe kuungana, utengano alianzisha nani? na kwa faida ya nani?........mbona babu zetu walimwabudu Mungu wao toka zamani kabla ya ujio wa wazungu.

Kwa ujumla dini imechangia kwa kiasi kikubwa sana katika kudumisha mtu kimawazo na kumfanya atumie fahamu tu kwa hiyo katika kumkomboa mtu kimawazo sharti suala la dini litupiwe jicho kali fasihi inazidi kuona jicho lake.

(d)Kiutamaduni.

Kwa ujumla utamaduni wanchi zilizotawaliwa na ukoloni umeathiriwa sana na ukoloni huo watu wa nchi hizo wanazipoteza kidogo kidogo thamani za utamaduni zao.Katika fasihi ya Kiswahili ukweli huu wa mambo yameoneshwa  katika kitabu cha “Njozi za Usiku” mwandishi wa riwaya hii ameelezea namna vijana wote hasa waliosoma hawataki kabisa kusikia kuhusu mila na desturi zao (uk 51).Hadi leo vijana wengi wakiwa kwao (vijijini) na ikatokea kwamba kuna ngoma za kienyeji zinachezwa wao husimama mbali au kando wakitazama kwa dharau mambo yanayotendeka mbele yao.Wanaamini kabisa kuwa ngoma hizo ni za kishenzi ngoma ambazo zinafaa kuchezwa na watu wasiosoma watu wasio staarabika.

Katika riwaya ya “Kichwa maji” mwandishi ameonesha jinsi isivyo  kawaida kwa msomi au watu wenye cheo serikalini kucheza ngoma za kienyeji lakini vijana hao hao mwanzoni wasomi wenye mwazo ya kisiasa wakisikia sehemu fulani kuna mziki au disko watajitahidi sana ili wasikose kufika huko.Kwa sasa kuna mtindo mwingine wa kupaka madawa ya kujichubua ngozi waonekane weupe na wengine huvaa nywele za bandia au maiti ili kuficha nywele zao za kipilipili.Huu wote ni utumwa wa kimawazo kwa upande fulani watu hawa wanaamini kuwa uzungu ndilo shina la maarifa, watu hawa hawajui kwamba kuna wazungu wengine ni maskini zaidi hata kuliko sisi wenyewe.Hivyo ili tujikomboe katika nyanja hizi ni lazima tuondoe ubinafsi, uroho wa madaraka na ulevi wa madaraka hapa nchini.

KAZI ZA FASIHI KATIKA MIFUMO MBALIMBALI

Kwa kuwa mwanadamu ni alfa na Omega wa Fasihi ni dhahiri kuwa maendeleo yake yanahusiana na maendeleo ya fasihi.Hata hivyo sio kila maendeleo huwa na mafanikio mazuri na hivyo si kila fasihi inatoa mawazo mema.Fasihi kama zao la jamii huenda sambamba na maendeleo  ya jamii yanayotokana na kazi  na fasihi hujitokeza katika Nyanja zote za kimaendeleo ziwe za kisiasa,kiuchumi,na kiutamaduni.Safari ndefu ya kimaendeleo imo katika mifumo mitano (5) ya uzalishaji mali.Mifumo hiyo ni kama ifuatayo:

  Fasihi katika mfumo wa Ujima

 Huu ni mfumo wa mwanzo kabisa wa maisha ya binadamu.Fasihi ya kipindi hiki ilikuwa fasihi ya uzalishaji mali.Mfumo wa ujima haukuwa na matabaka ya watu hivyo fasihi ya wakati huo ilijishughulisha na manufaa na maslahi ya watu wote Katika jamii.Katika mfumo huu fasihi na sanaa ni vitu vilivyokuwa vimefungamana na mahitaji ya kukidhi haja ya lazima ya watu. Fasihi katika kipindi hiki ililea amali za jamii ambazo zilikuwa  ni KAZI na USAWA yaani Fasihi ililinganishwa na kazi.Hata hivyo kutokana na uduni wa uvumbuzi wa kisayansi na kiteknolojia,Fasihi ya wakati huo iliilea jamii katika jamii katika kutawaliwa na nguvu za jamii na mazingira.Katika kipindi hiki fasihi haikuwa kitu cha anasa.Mazingira ya wakati huo yalikuwa ya kiuhasama sana,hayakuruhusu kuwepo na anasa ya aina yeyote ile.Kutokana na mazingira hayo Fasihi ilizuka kuwa silaha mojawapo ya mapambano hayo.

  Fasihi katika mfumo wa Utumwa,

Mfumo huu ulitawaliwa na utabaka ambapo kulikuwa na mabwana na watumwa wao.Mfumo huu uliruhusu baadhi ya watu kuishi kwa jasho la wengine.Watu hao waliishi maisha ya anasa kutokana na ziada ya mali iliyozalishwa na watumwa wao.Katika mfumo huu uzalishaji mali umewekwa migongoni mwa watu wa tabaka la chini la watwana.Katika shughuli za kisanaa,mfano upande wa ushairi ,watu wa matabaka ya mabwana waliwekewa  watwana na kuwaburudisha  kwa kuwaimbia nyimbo na mashairi.Fasihi nyingi zilikuwa zaile za kuwatukuza mabwana;zinazotukuza utumwa.Fasihi nyingi za wakati huu zilitumiwa ili kuendeleza itikadi za kibwana.

 Pia kulikuwa na fasihi inayopinga mfumo huu wa kinyonyaji.Watumwa wanaotumiwa kuwa vyombo vya kuzalisha mali,wanatunga visa,hadithi,mashairi na nyimbo za kupinga mfumo wa kitumwa.Mara nyingi  mabwana wenye watumwa iliwabidi wawasake na kuwatenganisha watumwa wenye historian a lugha moja iliyowaruhusu kutunga fasihi ya pamoja iliyelea hoja na hisi zao za kupinga unyonywaji huo.

Kugunduliwa kwa maandishi kulileta sura mpya kwa upande wa fasihi ya wakati huo.Uandishi ulikuwa kwa watu wa tabaka la mabwana tu;nao ulielekezwa katika kutoa kazi za fasihi zinazotetea maslahi ya tabaka hilo.Kutokana na ugunduzi wa maandishi watunzi walianza mfano kukaa na kupanga juu ya vina na mizani katika ushairi.Kalam na karatasi zilitumika keneza mitazamo na itikadi za kibwana.Falsafa na mitazamo ya kiulimwengu wakati huo ilielekezwa huko katika kuulinda na kuuhalalisha mfumo wa kitumwa.Kwa mfano,mwanafalsafa Aristotle,katika falsafa zake,alisisitiza na kuhalalisha utumwa kwa kueleza kuwa kuwa ilikuwa amri ya MUNGU kwamba watu wengine wawe watumwa na wengine wawe mabwana.

Hatimaye mfumo huu wa kitumwa ulianza kutetereka kwa mikinzano mbalimbali.Biashara ambayo hustawi sana katika hatua za mwanzo za mfumo huu zilianza kufilisika .Wakati huo huo watumwa hujizatiti na kupinga vikali sana utumwa wao.Watu ambao hapo awali walikuwa na mali zao chache kama vile mashamba na ambazo walinyang’anywa na mabwana wenye watumwa,nao waliungana pamoja na watumwa katika harakati za kuupinga utumwa.

Katika hatua hii ya kukata roho kwa mfumo huu wa kitumwa ,ulitumika kama chombo kimojawapo cha kiitikadi cha kupinga mfumo huo.Tanzu mbali mbali za fasihi kama vile hadithi,ushairi,nyimbo n.k zilielekezwa katika harakati hizo.

   Fasihi katika mfumo wa kikabaila (Kimwinyi)

Ni mfumo ambao uhusiano wa kitabaka  unakuwa kiwango cha juu kabisa.Tabaka tawala la makabaila linamiliki njia zote za uzalishaji mali yaani kiuchumi na kiutamaduni.Njia za kiuchumi hutawaliwa  kwa mbinu mbalimbali  za kukodisha mashamba.Mfano aliyekodishwa anapangiwa kutoa fungu kuba sana kwa mwenye shamba wakati wa mavuno.Mtwana wa wakati huu hutofautiani sana na mtumwa wa kipindi cha mfumo utumwa.Fasihi ya wakati huu anatawaliwa na falsafa zinazojaribu kuhalalisha uhusiano huo wa wenye mashamba na njia nyingine za uzalishaji mali na wale wasio na chochote isipokuwa jasho lao.Fasihi ya kipindi cha ukabaila iliweka msisitizo kuusu mapambo yasiyo na maana;msisitizo ambao unaathiri kazi ya fasihi pia.Mfano katika utenzi wa Al-Inkishafi(1810)mwandishi anasema;

   37. Nyumba zao mbake zikinawiri,

        Kwa taa za kowa na za sufuri,

        Masiku yakele kama nahari,

        Haiba na jaha iwazingiye.

                             

        38. Wapambiye sini ya kuteuwa,

               Na kula kikombe kinakishiwa,

              Kati watiziye kuzi za kowa,

               Katika mapambo yanawirije.

      Katika utenzi huu,Sayyid Abdallah A.Nassir anatuusia kuhusu maisha na ametumia lugha ya picha ya maisha ya uozo wa wafalme wa Pate kama kielelezo cha uzuri usio na kifani wa maisha ya hapa duniani.Halafu anaonyesha jinsi ambavyo maisha haya anayoyaona kuwa uzuri mwingi yanamalizikia katika kaburi ambako miili ya hao wafalme inakuwa chakula kikubwa cha funza.Uozo wa maisha ya mamwinyi wa pate  umeibua Fani na Maudhui ya Al-inkishafi (1810)

   Pia katika Utendi wa mwanakupona (1962) mwandishi anamuusia binti yake kuwa ajikubali kuwa pambo mbele ya mume wake.Anasema;

                  38.  Na kowa na kuisinga,

                          Na nyee zako kufunga,

                          Na asmini kutunga,

                          Na firashini kutia

              39     Nawe ipambe libasi

                       Ukae kama arusi,

                       Maguu tia kugesi,

                      N mikononi makoa.

            41. Pete sikose za ndani,

                   Hina sikome nyaani,

                   Wanda sitoe matoni,

                   Na inshini kuitia

Katika utendi huu mwandishi anamuasa mwanamke aweke na kuelekeza akili yote kwenye kujipamba ambapo kwa kufanya hivi kumemfanya mwanamke abaki katik nafasi duni sana katika jamii;nafasi ya chini ya kuonekana,kujiona na kujikubali kuwa pambo la kuufurahisha moyo na jicho pamoja na uchu wa mwanamume.

 Pia mfumo huu unamdanganya akubali kumtumikia na kumtii mume wake bila kumbishia wala kumjibu kwa lolote lile atakalosema.Mwanamke anaaswa kwamba amtii na amuogope mume wake;

                  28. Keti naye kwa adabu,

                         Usimtie ghadhabu,

                         Akinena simjibu,

                        Itahidi kunyamaa,

                    36. Mpumbaze apumbae,

                             Amriye sikatae,

                             Maovu kieta yeye,

                              Mungu atakulipa.

 Katika ubeti wa 36 wa utenzi huu inaonyesha wazi kuwa dini ilitumika kama taasisi kubwa ya kudumisha na kuhalalisha unyonyaji na mgawanyiko wa jamii katika matabaka ya watu.Katika utenzi huu,binti anausiwa kuwa afuate yote anayoambiwa na anayoamriwa  na mume wake kwani yote ni amri ya MUNGU.Hapa tunagundua athari za kitabaka zilizojikita katika dini na mafundisho yake.Athari hizo zinazidi kumdidimiza  na kumkandamiza zaidi na kumfanya mtu duni sana.

    Katika mfumo huu maisha huwa ya kibiashara na yaliyozingwa na imani kubwa juu ya pesa.Pesa  zinaanza kuabudiwa katika mfumo huu,nazo hujitokeza  katika nyuso mbalimbali za rundo la utajiri wa makabaila.Katikautenzi wa sundiata jambo hili linajitokeza waziwazi mwandishi anaelezea kuhusu utajiri wa wafalme kama vile Mansa Mussa.Mfumo huu wa kikabaila haukuendelea kuwapo muda wote. Mikinzano ambayo daima huwapo baina ya wanyonyaji na wanyonywaji ,pamoja na nguvu za vibwanyenye uchwara ambao walikwishaumbika katika harakati za kitabaka.Upande mmoja wa harakati  hizo walikuwepa wakulima wanyonywaji  pamoja na vibwanyenye ambao daima wamekuwa wakijitahidi kuangusha mfumo huu wa kikabaila ili badala yake wakite mizizi ya kibepari.Nguvu zote hizi za kiuchumi na kisiasa  hatimaye kuuangusha mfumo wa kikabaila.

 Katika kipindi hiki pia fasihi ilikuwa chombo kilichosaidia kuendeleza harakati za kuuangusha mfumo wa kikabaila wakati makabaila waliitumia fasihi kueneza na kuendeleza itikati zao za kikabaila,papohapo wanyonywaji nao pia walitunga fasihi yao inayoeleza hisia zao,taabu zao na umuhimu wa kujikomboa.Kwa wakulima fasihi yao ilikuwa ndiyo silaha ya kifasihi na kwa vibepari uchwara piawalikuwa na fasihi yao ya kupinga ukabaila na kutetea umuhimu wa kuwa na mfumo mpya wa maisha yaani mfumo wa kibepari.Mfano wa fasihi ya Kiswahili ya wakati huo ni kama vile; Utenzi wa fumo liyongo (1913) ambap awali utenzi huu ulielezwa kwa njia yam domo tu.Kwa watu wa tabaka la chini waliosimulia kisa hiki cha liyongo kilionekana kuwa cha kusifu ushujaa wa mtu huyo lakini papo hapo liyongo alikuwa mtetezi na mpenda watu wanyonge.

         Fasihi katika mfumo wa kibepari

Fasihi ni zao la jamii na hufungamana na mfumo wa maisha ya jamii na pia ulifungamana n mapambano ya kudumu dhidi ya mazingira ,yaani kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni.Katika mapambano hayo dhidi ya mazingira kulikuwa na mitazamo tofauti ya fasihi.Pia fasihi ilionekana kuwa ni silaha mojawapo kati ya silaha nyingi zilizotumiwa na tabaka moja kutetea maslahi yake kwenye mapambano ya kudumu ya kitabaka katika jamii

Katika ubepari kuna matabaka mawili ya watu yaani wenye mali wanaoshikilia rasilimali zote na wanyonge wasio na kitu.Fasihi ya kibepari ilielezea uzuri wa fedha kwa sababu pesa iliabudiwa sana katika mfumo huu.Waanii wa kipindi hiki ni wale walionuia kupata pesa,wasanii hawa walivaa uso wa udanganyifu huku tegemeo lao kubwa ni gunia la fedha,unyang’anyi na umalaya.Mfumo hu umefanikiwa kuwatenga waandishi na jamii zao.Wengi wametunga kazi zao za fasihi ambazo maudhui yake,dhamira na lengo lake pamoja na fani  kama vile Mzimu wa watu wa kale (1958),Kisima cha giningi (1958),Siri ya sufuri (1974),Duniani kuna watu (1973),Mwana wa Yungi hulewa (1976), na Kosa la Bwana Msa (1984) zaidi wasanii hawa walishighulikia suala la kusisimua msomaji na kumpumbaza kwa visa vya upelelezi.Fasihi ya kibepari iliifumba macho jamii isiione machungu  yanayoisakama jamii.Fasihi hii huwafumba macho watu (jamii) ili wasione udanganyifu ulioshamiri katika jamii hiyo.Huwaficha wagandamizaji na kuwapa nguvu za kumiliki jamii kisiasa ,kiuchumi,na kiutamaduni ili kuendeleza matabaka yanayo wanufaisha wachache.

 Fasihi ya kibepari haikomboi watu kimawazo ili waweze kuchambua na kutambua jamii yao kwa jicho pevu.Haiwachochei wanaogandamizwa kukataa machungu yanayosababisha na wagandamizaji wachache.Katika mfumo huu fani huwa kubwa kuliko maudhui yaliyopatikana humo.Kazi a fasihi iliyo nzuri ni ile ambayo fani na maudhui huwa katika uwiano ulio sawa.Fani isaidie kuyaweka maudhui katika hali nzuri ya kueleweka kwa jamii.

 Fasihi katika mfumo wa kijamaa

Mfumo huu huu ulibuniwa na Marx na Angels ambao walidai kuwa mfumo huu utatetea na kuleta kheri kwa umma.Fasihi ya mfumo huu itakuwa ya kunufaisha umma na kulinda amali na hali ya jamii.Matunda ya kazi huwa kwa faida ya wote.Usawa,utu na kuheshimiwa ndiyo msingi wa fasihi ya kijamaa.Fasihi ya kijamaa ni ya jamii nzima ambapo huiangalia jamii kisiasa,kiuchumi na kiutamaduni.Huyamulika matatizo ya jamii.Ni chombo cha kuunganisha,kuadibu,kuhimiza,kuongoza na kushauri jamii katika lake la kufuta unyonge na uchafu unaoikabili jamii.

 Fani na maudhui katika fasihi ya kijamaa ni vitu ambavyo hufungamana kwa mtazamo wa jumla.Fasihi lazima iwe wazi ili watu wa ngazi zote waweze kuelewa na kuzichukua fikra nzuri zilizomo.Uhuru wa kuikosoa na kuichambua jamii ni wazi kwa fasihi hii,tofauti na fasihi ya kibwenyenye ambayo uhuru huu haupo.Hivyo basi, fasihi iliyo ya kweli ni ile inayoelewesha umma katika mapambano yake dhidi ya mazingira,kuikosoa jamii,na kuielekeza jamii katika ukombozi wa kweli.Fasihi ya dhati ni sharti iendeleze shabaha zilizofikiwa na umma yaani wakulima na wafanyakazi.

 MADA NDOGO-3; UHURUWA MWANDISHI/MTUNZI WA KAZI ZA KIFASIHI

Dhana ya uhuru wa mwandishi ni pana sana na inatazamwa kwa kuangalia vipengele kadhaa kama ifuatavyo:

    Mosi,uhuru wa mwandishi uko katika utashi,Bila utashi mwandishi atakuwa mwoga na mwepesi wa kukata tamaa.Atayumbishwa haraka kutoka kwenye msingi wa falsafa yake na Imani aliyo nayo juu ya mabadiliko yatokeayo katika jamii.Makombora ya wahakiki na wanasiasa huweza kumyumbisha, lakini kwa mwandishi mwenye utashi makombora hayo humkomaza.

Baadhi ya waandishi walioonyesha utashi wao katika Afrika ni ‘Ole Soyinka na Ngugi wa Thiongowaandishi hawa wameshambuliwa sana na wahakiki, lakini misimamo yao ni ile ile, pia wamewahi kufungwa na walipotoka kifungoni hawakubadili misimamo yao na wamekuwa hivyo kwa sababu ya utashi wa falsafa zao katika fasihi ya kiswahili, waandishi wenye utashi wapo na msingi wa kuwepo kwao ni kutoyumbishwa na matamshi ya jukwaani na wahakiki ambao hawajapevuka.

Pili,uhuru wa mwandishi umo katika kuwa na falsafa moja inayoeleweka, Falsafa ifanyayo  maandishi ya mwandishi moja yawe na kitu kijulikanacho kama lengo.Waandishi waliotajwa hapo juu yaani Ole Sanyika na Ngugi wa Thiongo ndio wanaongoza kuwa na falsafa zao zinazojulikana. Katika fasihi ya Kiswahili tunaona waandishi wachache wenye falsafa zao inayojulikana wengi tulio nao wanaandika kufuatana na jambo fulani au tukio la wakati huo bila kulinganisha leo ataandika juu ya mapenzi, kesho juu ya upelelezi na kesho kutwa mapinduzi mwishowe anakuwa na orodha ndefu ya vitabu visivyokuwa na lengo.Waandishi wachache tulio nao ambao wameelekea kuwa na falsafa inayoongoza maandishi yao ni kamaShaban Robert, G.Kezilahabi na Mohamedi Suleiman.Bila kuwa na falsafa maalumu ni rahisi  sana mwandishi kuyumbishwa.

Tatu,uhuru wa mwandishi umo katika kuitawala vema Sanaa yake,kama unaandika riwaya na hujui misingi ya Sanaa ya aina hiyo atajikuta katika kikwazo,utajikuta uhuru wa kisanaa unaweza kujaribu, lakini kazi utakayoitoa itakuwa hafifu.Kazi nzuri ya kisanaa ni ile inayounganisha vema ubunifu na uhalisia.Mwandishi akielemea sana katika ubunifu anazua matatizo mengine kazi ngumu aliyonayo mwandishi ni katika kupata barabara msitari huo.Mwandishi mwenye vitabu vingi anaweza kuwa na kitabu kimoja tu kilichoupatia vema mstari huo. Katika fasihi ya Kiswahili waandishi walioupatia msitari huo tunao ni kama vile Ebraim Hussein,Penina Mhando,Mohamed Suleiman, C.G Mng’ong’o na J.A.Safari.Msanii anayeweza kuitawala  vema Sanaa yake anaunganisha vizuri Sanaa na maudhui yake.

Mwisho, uhuru wa mwandishi umo katika lugha anayotumia,ili msanii atawale vema Sanaa yake nilazima ajue lugha anayotumia.Lugha ndicho kiungo maalumu kati ya Sanaa na kazi ya kifasihi mwandishi kama hajui vema lugha anayotumia atajikuta hana uhuru wa kukisema anachotaka kwa hiyo lugha ndiyo nguzo ya nne katika uhuru wa mwandishi, waandishi wa Kiswahili  waliokwisha kutajwa wanakitawala Kiswahili sanifu,Kiswahili sanifu ndiyo msingi wa fasihi ya Kiswahili.

Ni kweli kuna uhuru wa mwandishi?

Uhuru wa mwandishi ni nini?

Ni ile hali ya mwandishi wa fasihi kuwa huru na wazi katika kutoa mawazo au hisia zake kwa jamii.Ni uhuru wa kuandika na kulikosoa tabaka lolote katika jamii bila kupata matatizo yoyote.

Mwandisihi ni nani?

Ni mtu yoyote atumiaye muda wake mwingi  kuandika na kuzungumzia jamii yake kwa njia ya maandishi.

Je kuna uhuru wa mwandishi?

Kwa ujumla uhuru wa mwandishi ni uhuru ikiwa hakufaulu kudhuru tabaka tawala hii ni kwa sababu suala la uhuru wa mwandishi ni la kitabaka na lilianza pale jamii ilipogawanyika katika matabaka kwa maana hii uhuru wa mwandishi unaamuliwa na tabaka tawala

Kuanzia enzi za utumwa, maandishi ya liyovumbuliwa katika  fasihi andishi ya mwanzo ilikuwa ya wateule wachache tu na wenye vyeo vyao.Hao mabwana, wamwinyi na mabepari walihakikisha kila mbinu inatumika ikiwemo ya udhibiti wa maandishi ili kuendeleza na kulinda utawala wao.

Naye B.Goya (1974-78)anasema kuwa mwandishi hana uhuru kwa vyovyote vile kwa sababu yeye ni tokeo la jamii Fulani, kila jamii ina mipaka yake ambayo mtu hatakiwi kukiuka kwa vyovyote vile mwandishi huyu amebanwa na mipaka hiyo asivuke.Pindi avukapo mipaka hiyo atapambana na jamii hiyo (tabaka tawala) vitabu vya mwandishi huyo vitapigwa marufuku au vitabu vikitolewa havitanunuliwa au serikali itavikusanya na kuvifanyia mipango mwingine. Katika Afrika  kuna mifano mingi ya udhibiti wa waandishi mfano mzuri ni mwandishi maarufu wa Kenya Ngugi wa Thiongo ambaye kazi zake hasa ya “Ngaahika Ndeenda”(I will marry when I want)- Nitaolewa Nitakapotaka, ilimgombanisha na vyombo vya dola hadi akawekwa kizuizini, Ngugi ni mwandishi wa kwanza kufichua siri za mfumo wa kibepari kwa watu wanyonge aliliuzi tabaka tawala la jamii yake ambalo halikusita kutumia udhibiti na vyombo vyake vya Mabavu.

Baada ya uhuru vitabu vingi sana viliandikwa kwa kudhibitisha maandishi mbalimbali uliojitokeza waziwazi E.Kazilabialiandika riwaya “Rosa mistika”(1971),kitabu hiki kilipigwa marufuku kisitumike mashuleni na wala kisiuzwe waziwazi madukani.Ilidaiwa na waliokipiga marufuku kuwa kilikiuka maadili ya jamii kwa kueleza mambo ya aibu kwa wazi.Sura ya kumi ndiyo hasa ilitolewa mfano wa uchafu wa kitabu hiki.Udhibiti huo ulifanywa na Wizara ya Elimu na ulizusha maswali mengi kwa wasomaji.Wasomaji walianza kujiuliza, Je si kweli uchafu uelezwao katika “Rosa mistika” umo ndani ya jamii ya Tanzania? Je upotofu na uongozi mbaya ulifuchuliwa na riwaya hiyo hii si upo kati yetu? Kwa baadhi ya wasomaji ilielekea kuwa suala la uchafu wa maelezo yatokeayo kitandani baina ya wakuu wa chuo na wanafunzi wao lilitumika kama kisingizio tu cha kudhibiti ukweli wa masuala mengine nyeti yaliyowagusa viongozi yaliyowakilishwa na watu kama vile Bwana Maendeleo Deogratiusanayeshiriki katika kuwaharibu vijana.

Vitabu vingine ambavyo havieleweki vinasema nini, maudhui, falsafa na ujumbe wa mwandishi nimashetani(E.Hussein)“Aliyeonja Pepo”(F.Topan) na “Ayubu” Paukwa theatre Association.Na hivi viko kwa kukwepa mkono mrefu wa tabaka tawala.

DHIMA YA UHURU WA MWANDISHI.

·       Mwandishi atakuwa huru kuikosoa jamii au tabaka lolote litakaloenda kinyume nautaratibu wa jamii bila matatizo.Mwandishi atakuwa huru kuonyesha dhuluma, ukatili na ujangili unaofanywa katika jamii na tabaka lolote bila matatizo yoyote.

·       Kukiwa na uhuru wa mwandishi, msanii atakuwa na falsafa inayoeleweka pamoja na utashiwake.Hii itamfanya mwandishi awe na msimamo unaoeleweka.Msimamo  wake utamsaidia kuifundisha na kuielimisha jamii bila uoga.Ataijiulisha jamii hali yake na ataonesha jamii njia za kufikia haja na kutatua matatizo ya jamii bila uoga

·       Mwandishi atakuwa huru kutoa mwongozo katika jamii kwa kuikomboa jamii kutoka katika fikra mbovu za kugandamizwa,kunyonywa na kuonewa na tabaka tawala ili jamii ipate haki na heshima bila woga wa kuliondoa tabaka ambalo ndilo lenye mamlaka yote katika jamii.

·       Uandishi wa kikasuku utapungua, waandishi au wasanii huacha tabia ya kuwa vipaza sauti vya tabaka fulani katika jamii, wasanii makasuku huandika mambo bila kufikiri na kurudiarudia  mawazo yaliyokwisha semwa na wanasiasa majukwaani bila fikra mpya kwa hali hii hupotosha jamii.Hivyo kunapokuwa na uhuru wa mwandishi wa kutosha hali hii haiwezi kutokea kwa sababu mwandishi ataandika mambo mbalimbali yanayojitokeza katika jamii na hataweza kujikomba au kujipendekeza kwa tabaka tawala lenye mamlaka yote katika jamii.

·       Kunapokuwa na uhuru wa mwandishi fasihi inakuwa chombo cha kuikomboa jamii kiuchumi,kisiasa, kiutamaduni na kifikra (kimawazo). katika jamii ya kitabaka fasihi ni mali ya tabaka tawala na hutumia fasihi kutetea na kulinda maslahi yao.Hivyo inapokuwa mali ya jamii nzima inatumiwa na jamii hiyo katika kuwakomboa wanajamii wote.

·       Kunapokuwa na uhuru wa mwandishi, mwandishi anakuwa huru kuichokoza na kuisukasuka (kuichochea) jamii bila matatizo yeyote. Mwandishi atachokoza jamii ya wakulima na wafanyakazi kufikiri ili waweze kulichunguza tabaka tawala kwa jicho pevu na kutoa hadharani uozo uliopo katika kunyonywa, kupuuzwa,kuonewa, kugandamizwa na kunyanyaswa na tabaka tawala

·       Mwandishi atakuwa huru kuelimisha na kuishauri jamii katika mambo muhimu yanayojitokeza katika jamii bila woga.Mwandishi ataishauri jamii kuhusiana na mambo kama vile afya, elimu na ichague mambo gani yanafaa kuhifadhiwa na yapi hayafai vile vile msanii anakuwa huru kuirekebisha jamii bila woga kwa kuangalia yapi ni mazuri na yapi ni mabovu yanayotendeka katika jamii 

MADA NDOGO-4;MASUALA YA KIITIKADI NA DHANA YA UDHAMINI KATIKA KAZI ZA FASIHI

Maana ya Itikadi

Itikadi ni Imani ya watu au jamii fulani juu ya kitu fulani. Itikadi kisiasa ni mfumo wa mawazo na Imani ambao umewekwa na tabaka tawala/ tawaliwa au tabaka lolote lenye nguvu katika jamii inayohusika ikiwa na lengo la kulinda, kutetea na kuendekeza matakwa na maslahi yake. Utaratibu huo unaambatana na umilikaji wa njia kuu za uchumi na umilikaji wa mapato ya ziada yatokanayo na jasho la wazalishaji mali hizo, nyenzo za kitaaluma kama vile elimu ni nyenzo zisaidia kuimarisha itikadi kama vile dini vinatumika kutetea utaratibu uliowekwa na tabaka tawala.

Kimsingi kuna mitazamo miwili ya kiitikadi:-

i)                  Itikadi inayotetea na kulinda maslahi ya watu wchache tu katika jamii (utumwa, ukabaila na ubepari)

ii)               Itikadi inayotetea na kulinda maslahi na matakwa ya watu wengi katika jamii (ujima na ukomunisti).

Vile vile tunapojadili juu ya itikadi katika fasihi na usemi kwa ujumla pia tunaongelea juu ya utabaka uliopo katika jamii inayohusika . Kuna matabaka ya aina mbili:-

a)   Tabaka tawala

b)  Tabaka tawaliwa

·       Tabaka tawala linamiliki vyombo vya dola na kwa kutumia vyombo hivyo na kwa kutumia waandishi, tabaka tawala linaunda, linaendeleza na kutetea maslahi yake.Vile vile tabaka tawala lina nguvu za kiakili na za kielimu kwa manufaa yao. Mwandishi kwa ujumla hawezi kuepukana na mfumo huo wa kitabaka. Tabaka fulani huwadhamini waandishi kwa njia mbali mbali.

 UDHAMINI

Ni hali ya watu au shirika fulani kutoa fedha kwa ajili ya kugharamia kitu fulani . Mdhamini au wadhamini ni kundi la watu wenye shabaha zinazofanana wenye kusimama kama ufadhili wa mradi fulani. Katika fasihi hawa ni wale wanaosimamia makundi maalumu kipropaganda na kiitikadi.

AINA ZA UDHAMINI

Kuna udhamini wa aina mbili:-

i)                  Udhamini wa ushawishi

ii)               Udamini wa nguvu

Ø UDHAMINI WA USHAWISHI

Ni aina ya udhamini ambao mdhamini huwashawishi na kuwanunua waandishi au wasanii. Matokeo yake ni kwamba msanii anafungwa na matakwa ya mdhamini.

Ø UDHAMINI WA NGUVU

Huu ni udhamini unaotumia vyombo vya dola kama vile jeshi, polisi, magereza kumdhamini mtunzi au mwandishi n.k.Hakuna hiari katika udhamini wa nguvu, kila kitu kinaendeshwa kama vile mashine tu. Kwa ujumla mwandishi akidhaminiwa kwa nguvu za serikali huwa kama kasuku aimbaye na kuutukuza mfumo wa maisha uliopo katika jamii hata kama roho na moyo wake viko mbali sana na mfumo huo. Lakini msanii anapodhaminiwa kutetea umma, lazima kutakuwa na madhara yake katika jamii yake inayohusika.

Mwandishi wa fasihi katika kila nchi atakuwa na udhamini unaolingana na mazingira yake kwa mfano katika nchi ya Tanzania, mwandishi anaweza kuandika kwa udhamini wa jamii yake inayohusika.Mdhamini anaweza kuwa mtu binafsi mwenye fedha, shirika, chombo cha serikali, chama fulani au kundi la mataifa kwa ushirikiano. Pia mdhamini ni mwakilishi wa wenye mamlaka juu yake, kwa mfano katika serikali yaTanzania chuo kikuu ni mwakilishi wa serikali na serikali ni mwakilishi wa tabaka tawala. Hivyo msanii anayedhaminiwa na chuo kikuu ambacho ni chombo cha serikali hatimaye anajikuta anafanya kazi ili kuendeleza maslahi ya tabaka tawala.

SABABU ZA UDHAMINI

Ø Uhaba wa fedha kwa waandishi za kuendeshea shughuli zao za uandishi katika uandishi wa kazi za fasihi. Pesa zinahitajika kwa ajili ya kununulia karatasi, kalamu, uchapaji n.k.

Ø Kulinda na kutetea maslahi yawadhamini wao. Hii inatokea zaidi kama mdhamini ni wa tabaka tawala. Kama tabaka linalo tawala ni la mabepari kazi za fasihi zitatetea tabaka hilo.

Ø Kujulikana au kuipendekeza. Baadhi ya waandishi hudhaminiwa kwasababu ya kutakakujulikaa na kwa upande mwingine mdhamini anawadhamini waandishi kwa lengo hilo.

Ø Kupata fedha za haraka. Hawa huandika vitabu vyenye kujaa wahusika wakuu, mafundi wa kufanya mahaba, kutumia madawa ya kulevya na kufanya mapenzi kwa kutumia mipira ya kiume na kike bila kujali staha utamaduni wa jamii yake. Mwandishi anachojali hapa ni pesa na sio matakwa ya jamii yake.

Ø Kulazimishwa na tabaka tawala. Waandishi hawa wanakubali udhamini huo kwa kuogopa udhabiti wa kazi zao na tabaka tawala. Waandishi hawa wakikataa udhamini huo kazi zao zitadhibitiwa na kupigwa marufuku zisisomwe au kuchapishwa kabisa.

               UMUHIMU WA UDHAMINI

·       Husaidia waandishi chipukizi katika kuchapisha kazi zao.

·       Husaidia waandishi katika kufanya utafiti wa mambo mbalimbali yatakiwayo katika Sanaa hiyo ya fasihi.

·       Husaidia jamii kupata kazi mbali mbali za kifasihi.

·       Husaidia kuleta ushindani wa ubora wa kazi katika soko la kazi za fasihi.

·       Husaidia kuinua vipaji hasa vya waandishi chipukizi.

 ATHARI ZA UDHAMINI

Ø Mwandishi anayedhaminiwa anatakiwa kuandika yale tu ambayo mdhamini wake anayataka. Msanii hatakuwa na uhuru wa kuandika kitu chochote na kwa njia anayotaka.

Ø Mapana ya uandishi wake kidata, kigiografia na kimaudhui huamuliwa na mdhamini nakutegemea mahitaji yake na kiwango cha fedha alichonacho mdhamini.

Ø Ufafanuzi wa data na maudhui ya kazi ya fasihi lazima ulingane na mtazamo wa itikadi ya mdhamini.Hii ina maana kuwa mwandishi wa kazi ya fasihi hawezi kufanya ufafanuzi wa data na maudhui mwenyewe bila kumshirikisha mdhamini.

Ø Matokeo ya uandishi wa kazi za fasihi mara nyingi ni mali ya mdhamini na hutumiakuendeleza maslahi yake mabayo sio lazima yalingane na malengo ya mwandishi.

Ø Wasanii au waandishi wengi kutokana na kudhaminiwa huanza kuandika kazi zao kwakupenda pesa hii huwafanya waandishi kuwa makasuku kwasababu ya kuandika yale tu yasemwayo na mdhamini wake bila kuyafanyia uchambuzi wa kina.

Ø Udhamini hukuza utabaka katika jamii, hapa tunakuwa na tabaka la wenye nacho (mdhamini) na tabaka la wasionacho (msanii) mdhamini humnyonya msanii.

Ø Kuzuka kwa fasihi pendwa (riwaya ya pendwa).Hapa waandishi huandika kazi zao kwa lengo la kupata pesa za haraka, huandika riwaya pendwa ambazo zina soko kubwa hapa nchini hasa kwa vijana na wakati huo huo riwaya hizo hazifunzi lolote jamii Zaidi ya kuburudisha.

Ø Huchochea rushwa, hii ni kwa sababu waandishi wengi wanataka udhamini huo na matokeo yake wale wanapata udhamini huo lazima watoe chochote (rushwa) kwa mdhamini.


Share This :
...