MASIGNCLEAN101

Muundowa Kirai katika lugha ya kiswahili

Muundowa  Kirai katika lugha ya kiswahili
citylab
Monday 1 February 2021

 

Wataalamu wengi wanakubaliana kwamba kirai ni kipashio cha mimuundo ambacho kinaundwa na
sehemu kuu mbili ambazo ni: (i) neno kuu; na(ii) kijalizo

Neno kuu ni nini?
Akitumia mfano wa ndoano, O’Grady (1996: 185) anaeleza kuwa vishazi hujengwa katika kiunzi
chenye viwango viwili kama inavyoonyeshwa katika kielelezo hiki hapa chini (msimbo K ukisimama
badala ya kirai):

KN KT KV KE KH ← kiwango cha kirai
׀ ׀ ׀ ׀ ׀
N T V E H ← kiwango cha neno

Anaendelea kusema kuwa kila kiwango cha muundo wa kirai kinaweza kufikiriwa kama ndoano
fulani ambapo vipashio vya aina aina vinaweza kupachikwa. Kiwango cha chini kabisa ni kwa ajili ya
neno ambalo
kwalo kirai ndio hujengwa – N kwa upande wa KN, T kwa upande wa KT, V kwa upande wa KV, E
kwa upande wa KE na H kwa upande wa KH. Kipashio hiki ndicho huitwa neno kuu. Kwa hiyo,
kutokana na maelezo ya O’Grady, tunaweza kusema kuwa Neno kuu ni neno linalotawala kirai
chote. Neno kuu linachukuliwa kuwa linatawala kirai kwa kuwa linaweza kutokea peke yake katika
kirai kama mifano ifuatayo invyoonyesha:


1) KN
N
(Anapenda) vitabu
(Watoto wamefanya) mtihani

2) KT
T
(viumbe hai wote) hula
(Simu yako) inaita


3) KV
V
(Huu ni mchezo) mgumu



4) KE
E
Wewe unapika) vizuri 
Share This :
...